Tayari umeshamaliza kusajili kampuni Brela na sasa unajiandaa kukamilisha taratibu za kupata TIN kutoka TRA na hatimaye leseni ya biashara ili kuanza rasmi biashara yako. Umeshikwa na shauku kubwa kusubiria siku kuu ambayo utakata keki kuashiria ufunguaji rasmi wa biashara yako. Lakini, Dudumizi inapenda kukukumbusha kuna kitu umekisahau kwenye orodha ya shughuli za kufanya, nacho ni usajili wa .co.tz domain.
Kumbuka, si lazima uwe na Website ndiyo usajili Domain, usajili wa domain unatakiwa kufanyika mapema ili kulinda jina lako hata kama haujaanza kulitumia. Sajili domain hapa.

Historia ya majina ya Website:

Kabla ya mwaka 1984 ambayo University of Wisconsin technicians walitengeneza seva za majina ya website(Name Server), hakukuwa na majina ya Website, watu walitumia namba tu, mfano, kama unataka kutembelea Website ya Dudumizi, ulitakiwa kuandika https://198.207.55.196. Hebu fikiria tungekwa tunaiandikaje kwenye Business card?
Mwaka 1985, majina ya Website kwa kutumia .com, .net na .org yalianza kutumika na watu kuanza kuachana na namba. Kwa kulitambua hilo, kwa tanzania, mchakato ulianza mwaka 1995 na hatimaye, TCRA iliuna tzNIC kama msimamizi mkuu wa .tz domaiin, na hatimaye, mwaka 2009, tzNIC ilianza rasmi kumanage majina ya .tz domain kupitia kwa mawakala wake, Dudumizi ikiwa mmoja wao.
Ingawa wapo watu wenye shauku ya kumiliki domain ya .co.tz lakini, kuna maswali au utata unaozunguka kichwani, hivyo, makala hii itasaidia kutatua maswali yanayoweza kujitokeza kuhusu .tz domain.

1. Je nitahitaji .tz pamoja na .com

Jibu la swali hili ni NDIYO au HAPANA, .tz ndiyo mpango mzima. Haijalishi unafanya biashara Tanzania pekee au dunia nzima, .tz itakufikisha huko na inatosha kabisa. Kumbuka, haijalishi unatumia kikoa cha .tz au .com, zote zitapatikanika dunia nzima. Tofauti tu, kwa kutumia .tz mtu anaweza kujua moja kwa moja hii ipo Tanzania bila hata kwenda kwenye mawasiliano.
Kuna woga au dhana ambayo ipo kwa wengi wetu ya kuhofia matumizi ya .co.tz inayopelekea kuamini kama .com ndiyo inayojulikana na watu. Google imeboresha sana upatikanaji wa Website bila kuathiriwa na kikoa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...