Marehemu Mzee Felician Makwaia

Ilikuwa siku, miezi na leo hii ni mwaka wa tatu tangu ulipotuacha kwa machungu mengi siku ile ya tarehe 30th May 2013 ukiwa Jaslok Hospital, India. Kimwili haupo nasi bali kiroho tupo nawe, Daima tunamshukuru Mungu kwa muda wote uliokuwa nasi, Sio tu kuwa Baba mwenye upendo bali kwa kuwa ulikuwa mtu wa pekee miongoni mwetu. Uliyebarikiwa kwa mambo mengi, ucheshi wako, hekima na busara zako, na juu ya yote hayo ulikuwa unafanya jambo kwa kusudi maalumu kwa kupenda usawa kwa kila binadamu, na kuwataka watoto wako tuwe na upendo na kutambua umuhimu wa elimu katika familia na jamii.

Tutaendelea kukumbuka na kufuata ushauri wako na mema mengi uliyotufundisha, na daima tutaendelea kukumbuka busara zako Baba na tutaendelea kukuenzi hadi tutakapo kutana tena paradiso.


Daima unakumbukwa sana na mke wako Mama Thecla Makwaia; watoto wako Stella Makwaia, Frank Makwaia, Robert Makwaia na Christopher Makwaia (MK), wajukuu zako Magdalen Christopher Makwaia pamoja na Madeleine Christopher Makwaia, unakumbukwa sana na ndugu zako, marafiki zako, majirani zako wote, wafanyakazi wenzako na Idara mbali mbali ulizowahi kufanyakazi kipindi cha uhai wako.


Tutakukumbuka daima Baba.


PUMZIKA KWA AMANI. AMEN.

*Misa ya kumbukumbu itafanyika tar 29/05/2016 saa 2.30 asubuhi katika kanisa la St. Maximilian Kolbe – Mwenge Afrika Sana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...