Sehemu wa Washiriki wa Majadiliano hayo ambayo yalijikita zaidi katika kuhakisha ni kwa namna gani serikali zinatekeleza  utoaji wa elimu  jumuishi ,  nyenye  kiwango bora  pasipo kumwacha yeyote nyuma, changamoto zake na nini kifanyike.

Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akizungumza jambo  na Waziri Mkuu wa  Norway, Mhe. Erna Solberg wakati wa  majadiliano kuhusu  utekelezaji wa  Lengo Namba Nne la Maendeleo  Endelevu kuhusu Elimu
Na Mwandishi Maalum, New York
Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania  imeanza kwa namna moja ama nyingine  utekelezaji wa  lengo namba Nne  ya Maendeleo  Endelevu kuhusu  Elimu la Maendeleo Endelevu (SDG4) kwa  kutoa  elimu   bure kuanzia shule  ya msingi hadi sekondari ikiwa ni  pamoja  na kuifanya  jumuishi kwa makundi  yote ya jamii wakiwamo  walemavu wa aina mbalimbali.

Hayo yameelezwa na   Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania  katika Umoja wa Matifa, Balozi Tuvako Manongi  wakati  wa majadiliano  kuhusu    utekelezaji wa  lengo   namba Nne ambalo ni  kati ya Malengo 17  ya Maendeleo Endelevu,  maarufu kama agenda 2030 yaliyopitishwa  mwezi  septemba mwaka jana  na viongozi wakuu  wa nchi na serikali.

Balozi Manongi alikuwa mmoja wa wazungumzaji wakuu katika  majadiliano hayo, ambayo yalimhusisha pia Waziri Mkuu wa Norway, Mhe. Erna Solberg na Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Bi. Irina Bakova na  yaliandaliwa kwa ushirikiano wa UNESCO na  UNICEF kama sehemu ya Mkutano wa  Kilele wa Kisiasa  wa Baraza   la Uchumi la Umoja wa Mataifa ( ECOSOC) unaoendelea hapa  Umoja wa Mataifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...