Sehemu wa Washiriki wa Majadiliano hayo ambayo yalijikita zaidi katika kuhakisha ni kwa namna gani serikali zinatekeleza utoaji wa elimu jumuishi , nyenye kiwango bora pasipo kumwacha yeyote nyuma, changamoto zake na nini kifanyike.
Na Mwandishi Maalum, New York
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeanza kwa namna moja ama nyingine utekelezaji wa lengo namba Nne ya Maendeleo Endelevu kuhusu Elimu la Maendeleo Endelevu (SDG4) kwa kutoa elimu bure kuanzia shule ya msingi hadi sekondari ikiwa ni pamoja na kuifanya jumuishi kwa makundi yote ya jamii wakiwamo walemavu wa aina mbalimbali.
Hayo yameelezwa na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Matifa, Balozi Tuvako Manongi wakati wa majadiliano kuhusu utekelezaji wa lengo namba Nne ambalo ni kati ya Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu, maarufu kama agenda 2030 yaliyopitishwa mwezi septemba mwaka jana na viongozi wakuu wa nchi na serikali.
Balozi Manongi alikuwa mmoja wa wazungumzaji wakuu katika majadiliano hayo, ambayo yalimhusisha pia Waziri Mkuu wa Norway, Mhe. Erna Solberg na Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Bi. Irina Bakova na yaliandaliwa kwa ushirikiano wa UNESCO na UNICEF kama sehemu ya Mkutano wa Kilele wa Kisiasa wa Baraza la Uchumi la Umoja wa Mataifa ( ECOSOC) unaoendelea hapa Umoja wa Mataifa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...