Rock City Marathon ilizinduliwa rasmi jana jijini Dar es Salaam huku wito ukitolewa kwa wadau wa mchezo wa riadha kote nchini kuhakikisha wanafanya jitihada za makusudi kuukomboa mchezo huo uliolipa taifa heshima miaka ya nyuma.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa mbio hizo kwa niaba ya Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo Bw Nape Nnauye,  Kaimu Mkurugenzi Idara ya Michezo wa Wizara hiyo Bw Alex Nkenyenge alisema kuna haja ya kuwepo kwa jitihada za makusudi miongoni mwa wadau wa mchezo huo ili kurejesha makali ya taifa katika riadha yaliyoonyeshwa miaka ya 1970 na 1980.

Kupitia mkurugenzi huyo Waziri Nape alitoa wito kwa wadau wa mchezo huo kuhakikisha wanashirikiana na serikali kuhakikisha changamoto zinazokwamisha mchezo huo zinatatuliwa ili kuwezesha uwepo wa maandalizi ya kutosha kwa wanamchezo huo.“Ndio maana nawapongeza waandaaji wa mbio hizi kwa kuwa wanashikiri moja kwa moja kukamilisha adhma yetu hii muhimu…kama serikali pia tunaahidi kuendelea kushirikiana nao,’’ alisema.

Akizungumza kwenye hafla Mratibu wa mbio hizo kutoka kampuni ya Capital Plus International, Bi Elizabeth Riziki alisema mbio hizo zinatarajiwa  kufanyika Septemba 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza zikihusisha wanariadha kutoka ndani na nje ya nchi ikiwemo baadhi ya nchi za Afrika, Ulaya na Marekani. Alisema mbio hizo zinazofanyika kwa mara ya nane mfululizo tangu zianze mwaka 2009 zinalenga kutambua na kuinua vipaji vya wanariadha nchini na pia kukuza utalii wa ndani kupitia sekta ya michezo.

“Rock City Marathon zitahusisha makundi matano yaani mbio za kilomita 21 kwa wanaume na wanawake, mbio za kilomita 5 kwa ngazi ya ‘corporate’, mbio za kilomita 3 kwa ajili ya walemavu, mbio za kilomita 3 tena kwa ajili ya wazee umri zaidi miaka 55 na kuendelea pamoja na mbio za kilomita 2 kwa ajili ya watoto umri kati ya miaka 7 hadi 19,’’ alitaja.

Alitaja  baadhi ya makampuni yaliyojitokeza kudhamini mbio hizo ikiwa ni pamoja na Freidkin Conservation Fund, African Wildlife Trust, Mwanza Hotel, Nyanza Bottlers Limited na kampuni ya Real PR Solution.

“ Pia mbio za mwaka huu zimeboreshwa zaidi kwa kuwa zitaambatana na uwepo wa majiko ya wachoma nyama ili kutoa fursa kwa washiriki kufurahia aina hiyo ya kitoweo pamoja na vyakula tofauti vyenye asili ya mkoa huo…ifahamike lengo la mbio hizi kukuza utalii wa ndani ,’’

Tunawaalika wadhamini waendelee kujitokeza kwa wingi ili kuzifanya mbio za mwaka huu kuwa bora zaidi,” alisema.Akizungumza kwenye hafla hiyo mdhamini mkuu wa mbio hizo  Bw Pratik Patel ambae ni Mkurugenzi Mtendaji wa mashirika ya Freidkin Conservation Fund( FCF) na African Wildlife Trust (AWT) alisema wameamua kuwa sehemu ya mbio hizo kwa kuwa zinaendana na mkakati wao kukuza utalii kwa kulinda maliasili.

“Tunafurahia kuwa sehemu yam bio hizi kwa kuwa lengo lake linaenda sambamba na agenda yetu ya kulinda maliasili na zaidi linaenda sambamba na kampeni yetu ya kupinga vita ujangili inayofahamika kama ‘Okoa Wanyama Wetu; Kataa Ujangili’. Alisema.

 Kaimu Mkurugenzi wa idara va Michezo Wizara ya  Habari, Sanaa na Michezo  Bw Alex Nkenyenge (alieshika mkasi) akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Rock City Marathon wakati wa hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es jana. Wanaoshuhudia ni pamoja na Mratibu wa mbio hizo kutoka kampuni ya Capital Plus International, Bi Elizabeth Riziki (wa kwanza kushoto)Mkurugenzi Mtendaji wa mashirika ya Freidkin Conservation Fund( FCF) na African Wildlife Trust (AWT), ambao ndio wadhamini wakuu wa mbiohizo Bw Pratik Patel (wa pili kulia), Bi Ombeni Savara katibu Mkuu Msaidizi chama cha Riadha Tanzania (wa kwanza kulia) na Joseph Kahama mwenyekiti wa maandalizi ya mbio hizo.
 Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mbio hizo Bw Joseph Kahama akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa mbio hizo.
 Mwanaridha mkongwe nchini Bw Juma Ikangaa akitoa nasaha zake kwenye hafla ya uzinduzi wa mbio hizo.
Mkurugenzi Mtendaji wa mashirika ya Freidkin Conservation Fund (FCF) na African Wildlife Trust (AWT), ambae ndio wadhamini wakuu wa mbio
 Kaimu Mkurugenzi wa idara va Michezo Wizara ya  Habari, Sanaa na Michezo  Bw Alex Nkenyenge akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi rock City Marathon.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...