RATIBA TU NI MUHALI,,HAYO MENGINE KWETU SI BAHARI?? 

Haji S Manara.  

 Kuna kurogwa na kujiroga,Kuna kufa na kujiua pia kulia na kuliliwa, Sisi watanzania hakika tupo ktk fungu la pili, fungu la kukosa , fungu mzigo, tunajiroga,tunajiua na tunaliliwa.

Hakika hatujui twataka nn, hatujui malengo yetu, lakini kubwa hatujui hata tutokapo wala tuendako, na leo naandika kitu kidogo tu kinachotushindwa kwenye soka letu, RATIBA

 Wakati wenzetu wanazungumzia  changamoto nzito na kubwa ktk maendeleo yao ya mchezo murua zaid duniani wa soka, Watanzania tunahangaika namna ya kupanga ratiba ya mechi zetu za ligi yetu na Kombe la Shirikisho, ratiba inayobadilishwa Kama nguo, tena mvaaji mwenyew ni mbunifu wa mavazi au mwanamitindo, ambae huvaa nguo tano Kwa siku.

Siku za nyuma niliwahi kuwaambia Clouds fm kuwa, iwapo ratiba ya Ligi kuu nchini isipopanguliwa ntatembea bila shati toka Mtaa Msimbazi hadi zilipo ofisi za TFF pale karume stadium,

Nilidhani Kwa kusena vile walau TFF na bodi ya Ligi wataona haya na kuhakikisha ratiba ya Ligi kuu haitabadilishwa tena, kumbe ndio kwanza wakubwa wameweka gundi masikioni, toka wakati ule ratiba ishafumuliwa Mara tatu, na leo hii imebadilishwa tena, Kwa kisinguzio kile kile, eti ratiba za Caf na za ligi zimeingiliana. 

 Ninajiuliza iwapo ratiba ya Ligi yetu ni muhali kuipanga,vipi kuhusu program nyingine za maendeleo? 

Itakuwaje kuhusu timu yetu ya taifa juu ya ndoto zetu za mchana wa jua kali? vipi kuhusiana na zile programu hewa za soka la vijana, watoto na wanawake?

 Hakika kwetu hayo ni sawa na bahari ya Mediterranean au bahari kuu ya hadithi za Alfu Leila uleila, hatuwezi ratiba tutaweza kwenda Afcon 2019? hatuwezi kupanga ratiba tutaweza kuwa na mipango madhubuti ya kuendeleza mchezo huu ambao yatajwa watu bilioni tatu duniani kote wanaushabikia? 

Kama tumerogwa aliyeturoga Kafa, hatuponi hadi Kiyama , tutakapokutana nae mchawi wetu. 

Nimalizie Kwa kuwapa mtihani mwingine TFF na bodi ya Ligi, iwapo Kama ratiba yao ya Ligi kuu na Kombe la shirikisho haitabadilishwa kuanzia sasa hadi mwisho wa msimu, ntamposa mlimbwende Wema Sepetu, na akikubali ntamuoa, akikataa ntatembea na boxer toka Nyumbani kwangu hadi TFF..

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...