Na Chris Lukosi
Napenda kuwashukuru sana Watanzania wote waishio UK kwa kujitolea kwa hali na mali wakati wa msiba wa Baba yangu
Pamoja na makubwa waliyonifanyia ni pale waliponichangia kwa kila mtu alichokua na nacho ambapo ilisaidia kwa kiasi kikubwa kukamilisha mazishi ya mzee wangu.
Lakini wana diaspora hawakuishia hapo. Leo hii Uongozi wa Tanzuk Diaspora (Watanzania Uingereza) wamenikabidhi hundi ya pesa tasilimu pounds £2,400 kama rambi rambi kutoka kwa uongozi wa Diaspora UK . Hizi ni tofauti na zile ambazo wana diaspora walinichangia kwa moyo mmoja moja kwa moja kwenye account yangu
Kwa kweli sina la kuwalipa zaidi ya asante, mliyonifanyia namuomba Mungu atuwezeshe tuwe na umoja huu wakati wote
UMOJA NI NGUVU...!
Mungu Awabariki Sana - AMINA
Chris akikabidhiwa ubani wake kutoka kwa Katibu Mkuu wa Diaspora UK Bw. Abraham Sangiwa nyumbani kwake Uingereza
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...