Bondia Mohamed Matumla anafanyiwa upasuaji wa kichwa muda huu baada ya ngumi aliyopigwa kuleta madhara kwenye kichwa chake na damu kubainika kuwa imevujia huku hali yake ikiwa nzuri
Taarifa zilizotufikia ni kuwa Vipimo vya CT scan vimeonyesha kuvuja kwa damu na imejikusanya sehemu moja na madaktari wanahangaikia kunusuru maisha ya mwanamasumbwi huyo ambaye hali yake si nzuri.
Operation ilichelewa kufanyika mapema kwa kuwa alihitajika kuongezewa damu, "tumefanikiwa kupata damu ameshaongezewa na akitoka chumba cha upasuaji ataongezewa damu nyingine"
Wapenzi na wadau wa ngumi kwa muda huu tumuombee DUWA mwenzetu operation yake ifanikiwe
SADICK & CO LTD ipo na mgonjwa toka aliposhuka kwenye ulingo na kusimamia matibabu yake yote
Tutaendelea kuwapa taarifa baada ya kutoka chumba cha upasuaji na hali yake itakavyokuwa inaendelea.
Promota STONE
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...