Bondia Mohamed Matumla anafanyiwa upasuaji wa kichwa muda huu baada ya ngumi aliyopigwa kuleta madhara kwenye kichwa chake na damu kubainika kuwa imevujia huku  hali yake ikiwa nzuri

Taarifa zilizotufikia ni kuwa Vipimo vya CT scan vimeonyesha kuvuja kwa damu na imejikusanya sehemu moja na madaktari wanahangaikia kunusuru maisha ya mwanamasumbwi huyo ambaye hali yake si nzuri.

Operation ilichelewa kufanyika mapema kwa kuwa alihitajika kuongezewa damu, "tumefanikiwa kupata damu ameshaongezewa na akitoka chumba cha upasuaji ataongezewa damu nyingine"

Wapenzi na wadau wa ngumi kwa muda huu tumuombee DUWA mwenzetu operation yake ifanikiwe

SADICK & CO LTD ipo na mgonjwa toka aliposhuka kwenye ulingo  na kusimamia matibabu yake yote

Tutaendelea kuwapa taarifa baada ya kutoka chumba cha upasuaji na hali yake itakavyokuwa inaendelea. 
Promota STONE                      

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...