Na Anthony John Glob Jamii.
 
 Chama cha walimu wanaofundisha masomo ya uraia wameitaka serikali kutokuchanganya maswala ya siasa na elimu kwakuwa yanawaathiri wanafunzi .

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa miradi wa chama hicho Goodluck Moleli amesema kuwa walimu wameonekana kutokushirikishwa katika maswala ya mabadiliko ya mitaala ya elimu na badala yake kutokujua mambo yanayo endelea katika mabadiliko ya mitaala hiyo ya elimu.

‘’Leo hii tumekutana hapa katika warsha hii ya walimu iliyoandaliwa na Ceta ilikujadili ni jinsi gani ya kuboresha elimu ya Tanzania Lakini tunaiomba Serikali ipunguze maswala ya kubadilisha mitaala ya elimu mara kwa mara kwakuwa wanafunzi wengi wanashidwa kufanya vizuri katika masomo yao’’ amesema Moleli

Mbali na hayo Mwalimu wa shule ya sekondari ya Kibweheri iliyopo Kibamba Sabrina Makafu amesema mtawala bado unashida na silabasi bado haziendani na vile tunavyo fundisha darasani mfano katika somo la kingereza unakuta tunacho fundisha sio kile kinacho toka katika mitihani.

‘’Inatupa sisi ugumu wa kufundisha kwakuwa tunayofunsisha hatuna uhakika kama ni hayo yatakayo letwa hivyo tunaiomba serikali kulifanyia kazi swala hili’’ amesema Mkafu.
Mkurugenzi wa miradi wa chama cha walimu wanaofundisha masomo ya uraia Googluck moleli akizungumza na waandishi wa habari mapema leo,jijini Dar.
Mwalimu wa shule ya sekondari sabrina makafu akizungza na waandishi wa habari jijini hapa leo hii
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...