Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje ya Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Rajabu (kushoto), akiongozana na wajumbe wengine wa kamati hiyo wakati wakiwasili katika eneo la mradi wa ujenzi wa kituo cha polisi, Oysterbay, leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje ya Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Rajabu (katikati), akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu baada ya kuwasili katika eneo la mradi unaoendelea wa Ujenzi wa Kituo cha Polisi, Oysterbay,leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mwigulu Nchemba.
Mtaalamu wa Majengo kutoka kampuni inayojenga Kituo cha Polisi Oysterbay, Mhandisi Fanuel Malekela, akitoa maelezo ya mchoro wa ujenzi wa kituo hicho kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje ya Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Rajabu (wapili kushoto),wakati kamati hiyo ilipotembelea ujenzi wa mradi huo.Wengine ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba(watatu kushoto) na Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu. Ziara hiyo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Kamishna wa Fedha wa Jeshi la Polisi, Albert Nyamhanga, akitoa maelezo ya mradi wa Ujenzi wa kituo cha Polisi,Oysterbay kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje ya Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Rajabu(watatu kulia), wapili kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba(kulia), akiwaongoza kutoka ndani ya jengo wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje ya Ulinzi na Usalama baada ya kumaliza kutembelea na kukagua maendeleo ya mradi wa Ujenzi wa kituo cha polisi,Oysterbay leo jijini Dar es Salaam.Huku sehemu kubwa ya mradi huo ikiwa imekamilika. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...