Katika
kuadhimisha Miaka 53 ya Muungano wa Tanzania tarehe 26 Aprili, 2017
Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutumia madaraka
aliyopewa chini ya Ibara ya 45(1)(d) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania ametoa msamaha kwa wafungwa wafuatao:-
Wafungwa
wote ambao baada ya punguzo la kawaida la moja ya tatu (1/3)
linalotolewa chini ya Kifungu 49(1) cha Sheria ya Magereza Sura ya 58,
wawe wametumikia nusu (½) ya vifungo vyao vilivyobaki, isipokuwa
wafungwa walioorodheshwa katika Ibara ya 2(i – xxi).
Wafungwa
wagonjwa wenye magonjwa kama UKIMWI, Kifua kikuu (TB) na Saratani
(Cancer) ambao wako kwenye “terminal stage”. Wafungwa hawa wathibitishwe
na Jopo la Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga
Mkuu wa Wilaya.
Wafungwa
wazee wenye umri wa miaka sabini (70) au zaidi. Umri huo uthibitishwe
na Jopo la Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu
wa Wilaya.
Wafungwa wa kike walioingia na mimba gerezani, pamoja na wale walioingia na watoto wanaonyonya na wasionyonya.
Wafungwa
wenye ulemavu wa mwili na akili (Physical disability and mental
disability). Ulemavu huo uthibitishwe na Jopo la Waganga chini ya
Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya.
Aidha, Msamaha huu wa Mheshimiwa Rais hautawahusu wafungwa wafuatao:-
Wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kunyongwa.
Wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kunyongwa na adhabu hiyo kubadilishwa kuwa kifungo cha maisha au kifungo gerezani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...