NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR. 

WAFUASI wa CCM wameshauriwa kutowachagua baadhi ya wanachama wenye kashfa na tabia za usaliti kuwa viongozi wa ngazi mbali mbali zinazowaniwa ndani ya chama na jumuiya zake hicho kupitia uchaguzi unaoendelea hivi sasa. 

Ushauri huo umetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho Zanzibar, Dkt. Abdalla Juma Saadala “ Mabodi” katika mwendelezo wa mafunzo elekezi ya kuwajengea uwezo watendaji na viongozi wa majimbo ya Mkoa wa Magharibi Unguja, ili waelewe kwa kina Mabadiliko ya Katiba ya CCM na kanuni mbali mbali yaliyofanyika hivi karibuni mjini Dodoma. 

Dkt. Mabodi alisema chama hicho ili kiendelee kuimarika ni lazima wanachama wake ambao ni waaminifu wafanye maamuzi magumu ya kuwaweka kando kwa njia ya Kidemokrasia baadhi ya wanachama wenye dalili na sifa za usaliti sambamba na kamati za maadili kuanzia ngazi za chini kuwafanyia vikao vya kikanuni kuwajadili na kuwapatia fursa za kujitetea endapo watakutwa na makosa wachukuliwe hatua kwa mujibu wa maelekezo ya Katiba na kanuzi za maadili. 

Pia Dkt. Mabodi alieleza kwamba lengo la kuchukua maamuzi hayo sio kuwaonea watu hao bali ni kukisafisha chama ili kibaki na wanachama waadilifu watakaokilinda na kukipigania katika mazingira yoyote hasa wakati wa chaguzi za chama na dola pamoja na vipindi mbali mbali vya misukosuko ya kisiasa nchini. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dkt. Abdalla Juma Saadala” Mabodi” akitoa ufafanuzi wa mabadiliko ya Katiba ya CCM yaliyofanyika mwaka 2017, kwa washiriki wa mafunzo elekezi ya kuwajengea uwezo ili waweze kuzikabili changamoto za uchaguzi wa chama na jumuiya zake. 
Mwasilishaji ambaye pia ni Afisa kutoka Makao Makuu ya CCM Dodoma, Nd.Alhaji Rajab Kundya akiwasilisha mada za Mabadiliko ya katiba ya CCM ya mwaka 2017, pamoja na maboresho ya kanuzi ya uchaguzi ya chama hicho. 
Ni baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia kwa makini mada zinazowasilishwa wakiwemo makatibu, wenyeviti , wajumbe wa kamati za siasa za ngazi za matawi hadi majimbo kwa chama na jumuiya zake, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mkoa wa Mjini Amani Unguja.(PICHA NA AFISI KUU CCM ZANZIBAR). 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...