Kamishna Jenerali wa
Idara ya Uhamiaji Dk. Anna P. Makakala wa kwanza kutoka kushoto akikagua vichochoro vinavyotumiwa na wahamiaji haramu kuingia
nchini katika kijiji cha Mugulika Kata ya Bwerenyange wilaya ya Karagwe Mkoani Kagera. Kamishna
Jenerali yuko mkoa wa Kagera kujionea shughuli zinazotekelezwa na Idara yake
mkoani humo.
Kamishna Jenerali wa Idara
ya Uhamiaji Dk. Anna P. Makakala wa kwanza kutoka kushoto akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya
ya Karagwe mkoa wa Kagera Godfrey
Mheluka watatu kutoka kulia katika
kijiji cha Muguluka Kata ya Bwerenyange
wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera.Kamishna Jenerali huyo amefanya ziara
katika Vipenyo vinavyotumiwa na wahamiaji haramu kutoka nchini nyingine kuingia
Tanzania.
Kamishna Jenerali wa Idara
ya Uhamiaji Dk. Anna P. Makakala wa nne kutoka kulia akiwa katika Mkutano wa
Hadhara na baadhi ya Wananchi (hawapo pichani) wa Kijiji cha Muguluka Kata ya
Bwerenyange wilaya ya Karagwe Mkoa
wa Kagera.Kamishna Jenerali huyo
amefanya ziara katika Vipenyo vinavyotumiwa na wahamiaji haramu kutoka nchini
nyingine kuingia Tanzania.
Baadhi ya Wananchi wa Kijiji
cha Muguluka Kata ya Bwerenyange wilaya ya Karagwe Mkoa wa
Kagera wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Idara ya Uhamiaji Dk. Anna P.
Makakala katika Mkutano wa Hadhara baina ya wanakijiji hao na Ujumbe huo wa
Idara ya Uhamiaji kutoka Makao Makuu ambapo katika Mkutano huo Dk.
Makakala alitoa wito kwa
wanakijiji hao kutowahifadhi
wahamiaji haramu kwenye makazi yao
sambamba na kuwataka kutoa taarifa kwenye vyombo vya dola pale wanapogundua
kuna mgeni asiyeeleweka na wanamtilia mashaka kwenye makazi yao.(Picha zote na
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...