Mwenyekiti wa Jumuiya ya serikali za mitaa nchini Tanzania (ALAT) na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Gulam Hafeez Mukadam ametoa msaada wa pampu ya maji na mifuko 10 ya saruji vyenye thamani ya shilingi milioni 2.5 kwa ajili ya kumaliza tatizo la maji katika kitongoji cha Mwamapalala kata ya Chibe katika manispaa ya Shinyanga. 

Mukadam amekabidhi msaada huo wa pampu ya maji na mifuko ya 10 ya saruji kwa diwani wa kata ya Chibe John Kisandu leo Ijumaa Novemba 17,2017 kwa ajili ya mradi wa maji katika mtaa wa Mwamapalala katika kata hiyo ambayo inakabiliwa na kukosekana kwa huduma ya maji. 

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo,Mukadam alisema hivi karibuni alitembelea kata ya Chibe,ndipo diwani wa kata hiyo akaomba msaada wa kutafutiwa pampu ya maji baada ya wananchi kujitolea kuchimba kisima kirefu. 

“Kutokana na ombi hilo,nimetafuta wafadhili na kupata msaada huu kutoka kwa Farana Hirji aliyenipatia fedha kwa niaba ya Roshan Chatur nikanunua pampu hii na saruji hii itakayotumika kukamilisha ujenzi wa kisima”,alieleza Gulam. 

“Kupitia msaada huu wananchi wa Chibe watapata huduma ya maji safi na salama kwani mhandisi wa maji wa manispaa amefika katika kisima hicho na kutuhakikishia kuwa maji hayo ni salama kwa matumizi ya binadamu”,alisema Mukadam. 
Zoezi la kushusha pampu ya maji kwenye gari likiendelea wakati Mwenyekiti wa Jumuiya ya serikali za mitaa nchini Tanzania (ALAT) na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Gulam Hafeez Mukadam akikabidhi pampu ya maji na mifuko 10 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa kisima kirefu cha maji katika kata ya Chibe manispaa ya Shinyanga- Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog 
Kaimu Mhandisi wa maji manispaa ya Shinyanga Nkinda Seni (wa nne kushoto) akishusha mabomba ya pampu ya maji.Katikati ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya serikali za mitaa nchini Tanzania (ALAT) na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Gulam Hafeez Mukadam 
Mwenyekiti wa Jumuiya ya serikali za mitaa nchini Tanzania (ALAT) na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Gulam Hafeez Mukadam akizungumza wakati wa kukabidhi pampu ya maji na mifuko ya saruji kwa diwani wa kata ya Chibe John Kisandu kwa ajili ya ujenzi wa kisima kirefu katika mtaa wa Mwamapalala. Kushoto ni pampu ya maji na mifuko ya saruji. 
Mwenyekiti wa Jumuiya ya serikali za mitaa nchini Tanzania (ALAT) na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Gulam Hafeez Mukadam akishikana mkono na diwani wa kata ya Chibe John Kisandu wakati wa akikabidhi pampu ya maji na mifuko ya saruji.Wa kwanza kulia ni Kaimu katibu mkuu ALAT,Abdallah Ngodu na Kaimu Mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga,Rajabu Masanche wakishuhudia zoezi la makabidhiano. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...