BENKI ya TPB imeingia kwenye makubaliano rasmi na kampuni ya Multichoice Tanzania inayotoa huduma za DStv ambapo wafanyakazi umma, wateja na hata wale wasio wateja sasa wanaweza kupata ving’amuzi vya DStv kwa mkopo na kisha kulipia kidogo kidogo.

Hafla hiyo ya kusaini makubaliano imefanyika leo jijini Dar es Salaam, ambapo Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya TPB Sabasaba Moshingi pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande wamesaini hazi za makubaliano. 

Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Sabasaba Moshingi alisema kwa sasa Watanzania wanaotaka kumiliki ving’amuzi vya DStv, wataweza kupata mkopo maalum kutoka TPB utakaowawezesha kufungiwa huduma za DStv na kisha kulipa kwa awamu kwa kati ya miezi mitatu hadi mwaka mmoja.

Alisema kuwa benki yake siku zote imekuwa ikijitahidi kubuni huduma mbalimbali kwa ajili ya kuwawezesha Watanzania wengi zaidi kupata huduma muhimu na pia katika kuboresha hali zao kiuchumi na kijamii. 
 Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya TPB Sabasaba Moshingi (kulia) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande (kushoto) wakibadilishana nyaraka za makubaliano mara baada ya kusaini.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya TPB Sabasaba Moshingi (kulia) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande (kushoto) wakisaini makubaliano ya ushirikiano, ambapo kwa sasa wafanyakazi umma, wateja na hata wale wasio wateja wanaweza kupata ving’amuzi vya DStv kwa mkopo na kisha kulipia kidogo kidogo. Nyuma yao ni mashahidi kutoka pambe zote mbili.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...