Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Sulemani Jafo amesema hatawavumilia wakurugenzi na wenyeviti wa kamati za fedha ambao hawatatoa fedha za maendeleo zinazotokana na mapato ya ndani ya halmashauri kulingana na bajeti zao.

Alitoa onyo hilo wakati akifungua kongamano la siku mbili la wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri juu ya uwajibikaji mamlaka za serikali za mitaa linalolenga kujadili nafasi ya mamlaka hizo katika kutekeleza azma ya serikali ya kufikia uchumi wa kati kupitia viwanda.

Jafo alisema wakurugenzi na wenyeviti hao wataondolewa katika nafasi zao endapo watashindwa kutoa fedha hizo ikiwa ni pamoja na asilimia tano za mapato ya ndani kwa vikundi vya vijana na wanawake.

“Wakarugenzi watakaoshindwa kutoa fedha katika mapato yao ya ndani hawatatosha katika kipindi cha utawala huu, umeipanga katika bajeti , umekusanya halafu vijana na akina mama hujawapelekea asilimia tano za mapato ya ndani, basi mkurugenzi utakuwa hutoshi”

 .WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Sulemani Jafo akizungumza katika kongamano la siku mbili  la wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri juu ya uwajibikaji mamlaka za serikali za mitaa linalolenga kujadili nafasi ya mamlaka hizo katika kutekeleza azma ya serikali ya kufikia uchumi wa kati kupitia viwanda lililofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mtenda wa Wajibu, Lodovick Utouh akizungumza juu madhumuni ya mkutano huo kwa wenyeviti wa halmashauri, Mameya na Wakurugenzi juu ya upangaji mikakati ya kuhudumia wananchi katika kongamano la siku mbili  la wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri juu ya uwajibikaji mamlaka za serikali za mitaa linalolenga kujadili nafasi ya mamlaka hizo katika kutekeleza azma ya serikali ya kufikia uchumi wa kati kupitia viwanda.
 Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa Taasisi ya Wajibu, Yona Kilaghane akizungumza juu maazimizio na utekelezaji wa wajibu maombi ya WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Sulemani Jafo katika kongamano la siku mbili  la wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri juu ya uwajibikaji mamlaka za serikali za mitaa linalolenga kujadili nafasi ya mamlaka hizo katika kutekeleza azma ya serikali ya kufikia uchumi wa kati kupitia viwanda.
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbulu, Hadson Kamoga akizungumza na waandishi wa habari juu utekelezaji wa maazimio yatakayotokana na kongamano hilo katika kongamano la siku mbili  la wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri juu ya uwajibikaji mamlaka za serikali za mitaa linalolenga kujadili nafasi ya mamlaka hizo katika kutekeleza azma ya serikali ya kufikia uchumi wa kati kupitia viwanda.
 Sehemu wenyeviti wa halmashauri, Mameya na Wakurugenzi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...