Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Dk. Juma Ali Malewa amepokea utambulisho wa Mwalimu wa Judo Shozy Yogi aliyekuja kumtembelea Makao Makuu ya Magereza jijini Dar es Salaam leo tarehe 06 December 2017.

Mwalimu Shozy Yogi alifika Makao Makuu ya Magereza akiambatana na kiongozi wa Japan International Cooperation Mr. Tsujimoto Makoto, Mkuu Msaidizi wa Kikosi Maalum cha kutuliza Ghasia Magerezani (KMKGM), Mrakibu Alli Uwesu na Msaidizi wa Mwalimu, Warder Oscarius.

Kamishna Jenerali Malewa aliupokea ugeni huo na kufanyanao mazungumzo ya jinsi mwalimu huyo ataendesha mafunzo hayo kwenye kambi ya KMKGM. Mwalimu Shozy Yogi aliwasili toka tarehe 17 November,2017 na amefika hapa Tanzania kwa mafunzo ya muda mrefu ya mchezo wa Judo kwenye kambi ya Kikosi Maalu cha Kutuliza Ghasia Magerezani (KMKGM)
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Dk. Juma Malewa akimsikiliza Kiongozi wa Japan Internation Cooperation (JICA) Mr. Tsujimoto Makoto alipomtembelea ofisini kwake.
Mwalimu wa mchezo wa Judo toka Japan, Shozy Yogi(Kushoto) akimsikiliza Kamishna Jenerali Dk. Juma Malewa (hayupo pichani) alipotembelea Makao Makuu ya Magereza. Kulia kwake ni kiongozi JICA ambaye amemleta Tanzania.
Kamishna Jenerali Dk. Juma Malewa(wa pili kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mwalimu Shozy Yogi(mwenye shati jeupe), Mr. Tsujimoto Makoto (mwenye suti nyeusi), Kamishna wa Utawala na Fedha(wa tatu kushoto). Wengine ni Mrakibu Mwandamizi Matilda Mlawa (wa kwanza kushoto), Mrakibu Alli Uwesu na Wdr Oscarius.
Kamishna Jenerali Dk. Juma Malewa akiagana na Mwalimu wa Judo Shozy Yogi ofisini kwake baada ya kufanya nae mazungumzo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...