Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe Deo Ndejembi, leo ameendelea na ziara katika kata ya Hogoro na vijiji vyote vitano vya Kata hiyo ambavyo ni Mkutani, Banyibanyi, Nyerere, Hogoro na Chamae. Hogoro ni kata ya 11 kati ya kata 22. 

Mpaka sasa DC Ndejembi amefanya ziara katika vijiji 44 kati ya 87 na Kata 11 kati ya 22. Lengo la ziara hii ni muendelezo wa kampeni yake ya Ondoa Njaa Kongwa( ONJAKO) iliyozinduliwa msimu huu wa Kilimo inayohimiza kilimo cha Mtama na Uwele ili kuhakikisha kuna usalama wa chakula wilayani. 

Vile vile akiwa katika vijiji hivyo DC Ndejembi husikiliza kero mbali mbali za wananchi na kutoa maagizo na maelekezo yenye kulenga kutatua kero hizo.Katika majukumu yake DC Ndejembi alikwisha tembelea kata zote 22, ila kwa sasa atatembelea Vijiji vyote 87 katika Wilaya ya Kongwa.
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe Deo Ndejembi, leo akizungumza na baadhi ya wananchi wa kata ya Hogoro,wilayani humo.Mh Deo ameendelea na ziara yake katika kata ya Hogoro na vijiji vyote vitano vya Kata hiyo ambavyo ni Mkutani, Banyibanyi, Nyerere, Hogoro na Chamae. Hogoro ni kata ya 11 kati ya kata 22.
Baadhi ya wananchi wakimsikilia Mkuu wa wilaya ya Kongwa,Mh Deo alipofanya ziara katika kata ya Hogoro na vijiji vyote vitano vya Kata hiyo ambavyo ni Mkutani, Banyibanyi, Nyerere, Hogoro na Chamae. Hogoro ni kata ya 11 kati ya kata 22. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...