Na Wankyo Gati, ARUSHA
Mkazi wa Mtaa wa Jamhuri kata ya Daraja Mbili Halmashauri ya Arusha
Mjini Mkoani hapa, Asha Hussein amewaomba Wananchi kumsadia Fedha za
Matibabu na kujikimu kimaisha kutokana na tatizo la Ugonjwa wa Utindio
wa Ubongo aliyepata Mtoto wake Abul Hussein (6).
Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwao , Mama Mzazi wa Mtoto huyo, alisema kuwa Mtoto
wake kwa kipindi cha Miaka Minne tangu kuzali kwake amekuwa akitumia
Mirija ya mipira wakati wa kula chakula kutokana na hali ya Ugonjwa
inayomkabili kwa sasa.
Aliongeza kuwa anawaomba Watanzania kunisaidia ili niweze kupata Matibatu ya Mtoto
sababu hali yake ni Mbaya sana nayakuuzunisha, suala la uchumi ni
ngumu hata kupata Fedha za kumshughulikia katika Matibabu limekuwa ni
shida kwa kweli”
Akizungumzia hali ya Ugonjwa kwa Masikitiko, Mama wa Mtoto huyo,
alisema kuwa kwa kipindi cha miaka Minne Mtoto wake amekuwa akiishi ya
kulishwa chakula kwa kutumia mirija, hali inayosababisha kutapika
kila Mara na wakati mwingine damu umtoka kutokana na mipira hiyo
kukaa tumboni kwa muda mrefu.
Alisema kuwa Mtoto huyo alipozaliwa alibainika kuwa alikuwa na tatizo
la kukakamaa na kutokuona vizuri ambapo alisema kitaalamu tatizo hilo,
linaitwa tatizo la utindio wa ubongo.
Kwaupande wake daktari bingwa Julius Msuya wa magonjwa ya kina mama na watoto
kutoka hospitali ya St Thomas Mkoani Arusha alisema kuwa hali hiyo
inatokana na uchelewaji wa mama kujifungua ambapo husababisha
kukosekana kwa hewa ya oksijeni katika ubongo wa mtoto na hivyo
kupelekea kupata matatizo mbalimbali ikiwemo kutokukomaa kwa viungo
vyake sanjari na kupata tatizo la utindio wa ubongo.
Msuya alisema kuwa wakati wakujifungu kwa kinamama ikitokea kama
kachelewa ndiyo matatizo kama hayo, yanamtokea Mtoto na kumsababishia
Madhara Makubwa .
Amina Salum ni Jirani, na yeye alitoa angalizo kwa wanawake na watoa
huduma wote wa hospitali hapa, Nchini kuwa makini ili kuepusha
upatikanaji wa watoto wa aina kama ya Abdul.
Alieleza kuwa Kumekuwepo na ongezeko la watoto wa aina hiyo katika
jamii hali ambayo imekuwa ikizua taharuki katika familia na wengine
kuhusisha ugonjwa huo na imani za kishirikina badala yake wakina mama
wajawazito wametakiwa kuchukua tahadhari juu ya suala hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...