Na Anthony Ishengoma.

Watoto wanaoishi katika Makao ya Taifa ya Watoto Kurasini wamefaidika na huduma ya Bima ya Afya kwa ajili ya matibabu yao baada ya shirika la Abbot Tanzania kuwezesha ufadhili wa huduma hiyo muhimu pamoja kuwafungulia akaunti za benki ili waweze kumudu kulipia upya wakati bima zao zinapofikia mwisho wa muda wake.

Shirika hili limekuwa mfadhili mkuu wa Makao ya Taifa ya watoto tangu mwaka 2001na limewezasha watoto wa kituo hiki kuhakikisha wanapata huduma mbalimbali ikiwemo ustawi wa watoto kiafya na huduma nyinginezo kama vyeti vya kuzaliwa, ujenzi wa mabweni pamoja na huduma za miundombinu ya kituo hicho.
Makao ya Taifa ya watoto wenye shida Kurasini yametembelewa na ujumbe maalum katoka Shirika linalofadhili kituo hiki la Abbot Tanzania ili kujionea Maendeleo ya shughuli za kituo hicho zinazofadhiliwa na shirika hilo.
Akiongea wakati wa kuwakaribisha wageni hao kituoni hapo, Kaimu  Kamishina wa Ustawi wa Jamii Simon Panga amesema Shirika la Abbot Tanzania limekuwa likitoa ifadhili wake kwa kituo hiki tangu mwaka 2001 na kufanikiwa kuleta mageuzi makubwa kwa Maendeleo ya kituo hiki.
 Wageni wa Makao ya Taifa ya Watoto Kurasini wakiangalia moja ya mradi wa ufugaji unaofadhiliwa na na Mfuko wa Abbot Tanzania katika Makao ya Taifa Dar es Salaam  aliye katikati ni Makamu wa Rais wa Mfuko wa Abbot  Bi. Jenna Daugherty.
 Baadhi ya watoto wa Makao ya Taifa ya Watoto wakiimba mbele ya wageni kutoka wafadhili wa Makao yao Abbot Tanzania pamoja na uongozi wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto jijini Dar es Salaam.
Mlezi wa Makao ya Taifa ya Watoto Bi. Beatrice Mugubilo akiongoza wageni wa Makao yake kuangalia maendeleo ya miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Abbot Tanzania.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...