Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akikata utepe kuzindua rasmi ofisi yake iliyojengwa kwenye mji wa Serikali jijini Dodoma kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi. Naibu Waziri, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) na Katibu Mkuu-Utumishi, Dkt. Laurean Ndumbaro wameshiriki tukio hilo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) wakifurahia uzinduzi wa ofisi yao iliyojengwa kwenye mji wa serikali jijini Dodoma, mara baada ya Mhe. Mkuchika kuzindua ofisi hiyo.
Mwonekano wa jengo la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora lililozinduliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) mara baada ya TBA kulikabidhi jengo hilo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akizungumza na watumishi na vyombo vya habari mara baada ya kuzindua rasmi ofisi yake iliyojengwa kwenye mji wa Serikali jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akiwa kwenye ofisi yake iliyopo kwenye mji wa Serikali jijini Dodoma mara baada ya kuizindua.
Mkurugenzi wa Ujenzi, Wakala ya Majengo Tanzania (TBA), Bw. Hamphrey Kilo akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa jengo la Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) (hayupo pichani) mara baada ya kumkadhi waziri huyo jengo hilo lililopo kwenye mji wa serikali jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akimkabidhi hati ya kiwanja mtumishi wake Bi. Zena Makaye, mara baada ya waziri huyo kuzindua rasmi ofisi yake iliyojengwa kwenye mji wa Serikali jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akimkabidhi hati ya kiwanja Mkurugenzi Msaidizi wa Ofisi yake Bw. Peter Mhimba, mara baada ya waziri huyo kuzindua rasmi ofisi yake iliyojengwa kwenye mji wa Serikali jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa ofisi yake mbele ya ofisi aliyoizindua ambayo imejengwa kwenye mji wa Serikali jijini Dodoma. Naibu Waziri, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) na Katibu Mkuu-Utumishi, Dkt. Laurean Ndumbaro ni miongoni mwa waliojumuika katika picha hiyo.



Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imeandika historia nchini ya kuwa taasisi ya kwanza kukabidhiwa jengo la ofisi yake na Wakala ya Majengo Tanzania (TBA) kwenye mji wa Serikali uliopo Mtumba jijini Dodoma, na jengo hilo kuzinduliwa rasmi na Waziri mwenye dhamana ya utumishi wa umma na utawala bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) kwa ajili ya kuanza kutoa huduma rasmi kwa wananchi na wadau wa masuala ya kiutumishi na utawala bora. 

Historia hiyo imeandikwa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, mara baada ya Mhe. Mkuchika kukabidhiwa rasmi jengo hilo na kukata utepe kuashiria uzinduzi wa huduma zitakazoanza kutolewa na ofisi yake kuanzia tarehe 02 Aprili, 2019 katika jengo hilo lililopo kwenye mji wa Serikali jijini Dodoma. 

Mhe. Mkuchika amesema ofisi yake imetekeleza kwa vitendo agizo la ujenzi wa ofisi katika mji wa serikali, na hatimaye kuandika historia ya kuwa taasisi ya kwanza kukamilisha ujenzi wa awamu ya kwanza na kuongeza kuwa, anaamini kwamba, ofisi yake ndio itakuwa ya kwanza kutoa huduma kwenye ofisi za wizara zinazojengwa katika mji huo wa Serikali. 

Mhe. Mkuchika amesisitiza kuwa, kuanzia tarehe 02 Aprili, 2019 yeye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na kurugenzi za Utawala Serikalini, Uendelezaji Sera na Taarifa za Utumishi na Mishahara kwa pamoja wataanza kutoa huduma katika ofisi hizo. 

‘Kuanzia Aprili 2, mtumishi au mwananchi mwenye uhitaji wa kumuona Waziri, Naibu Waziri,Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu afike katika ofisi za Utumishi mtumba ili aweze kuhudumiwa’, amefafanua Mhe. Mkuchika. 

Mhe. Mkuchika ameeleza kuwa, baada ya ofisi yake kuhamia, anaamini kwamba, ndani ya mwezi mmoja ujao wizara nyingi zitakuwa zimehamia rasmi na hatimaye wananchi na watumishi kutoka katika maeneo mbalimbali nchini watahitaji huduma ya usafiri kuja kwenye mji wa serikali ili kupata huduma, hivyo ametoa wito kwa mara nyingine tena kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri jijini Dodoma kuchangamkia fursa hiyo. 

Aidha, katika kuwawezesha watumishi wa ofisi yake kufanya kazi kwa ufanisi na kuwa karibu na ofisi iliyojengwa, Mhe. Mkuchika alitumia fursa hiyo kuwapatia hati za viwanja watumishi ambao ofisi imewarahisishia mchakato wa kununua viwanja vya serikali vilivyopo mtumba katika mji wa serikali ili watumishi hao wawe na makazi bora yatakayowawezesha kutekeleza majukumu yao kikamilifu. 

Mhe. Mkuchika ametoa rai kwa watumishi wote wa umma waliohamia jijini Dodoma, kuhakikisha wanajipatia viwanja vilivyopimwa na serikali na kujenga nyumba bora ili kuishi kwa staha na kulinda hadhi ya kuwa watumishi wa umma. 

Naye, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) ameishukuru Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa kukamilisha ujenzi kwa wakati na kwa kiwango bora na hatimaye kukabidhi ofisi rasmi ili ziweze kutoa huduma kwa wananchi. 

Dkt. Mwanjelwa amewashukuru na kuwapongeza watumishi wote wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa ushirikiano waliouonesha kwa menejimenti tangu mwanzo wa ujenzi mpaka ofisi imekamilika na kuwataka kuendelea na utamaduni huo wa ushirikiano. 

Kwa upande wake, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro amewashukuru watumishi wote wa ofisi yake kwa kushiriki kikamilifu katika kufanikisha ujenzi huo na amewapongeza watumishi hao kwa kutenga muda wao ili kushiriki katika zoezi la upandaji miti kwenye ofisi hiyo lililofanyika wakati ujenzi ukiendelea. 

Awali, akiwasilisha taarifa fupi ya ujenzi wa Ofisi hiyo ya Utumishi, Mkurugenzi wa Ujenzi, Wakala ya Majengo Tanzania (TBA), Bw. Hamphrey Kilo amesema, ujenzi ulianza rasmi mnamo tarehe 26 Disemba, 2018 na kutarajiwa kukamilika tarehe 22 Machi 2019, tarehe ambayo ndio wamekabidhi jengo ambalo kwa mujibu wa mkataba, kazi zote zilizoanishwa zimekamilika kwa kiwango bora. 


IMETOLEWA NA; 
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI 
OFISI YA RAIS (UTUMISHI) 
TAREHE 23 MACHI, 2019

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...