Na Eliud Rwechungura

Waziri wa Viwanda na Biashara, Prof. Kitila Mkumbo amekipongeza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kubuni utaratibu wa mashindano ya wanafunzi ya Ubunifu na Ujasiriamali inayofanyika kila mwaka.

Prof. Mkumbo ameyasema hayo Mei 08, 2021 katika siku ya wanafunzi ya Ubunifu na Ujasiriamali na fainali za Ubunifu na Ujasiriamali Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika ukumbi wa Nkrumah iliyokuwa na kauli mbiu inayosema “Badili Changamoto kuwa Fursa”

“Nakipongeza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kubuni utaratibu kama huu wa kusaidia kuibua na kukuza vipaji vya ubunifu vya vijana wetu katika kujibu matatizo ya jamii. Mimi hapa ni nyumbani, hivyo najisikia vizuri kuwepo hapa na kushiriki pamoja nayi” ameeleza Prof. Kilila Mkumbo

Prof. Kitila ameeleza kuwa ujuzi unaotakiwa katika soko la ajira na nini wanafunzi wafundishwe ili wakubalike katika soko la ajira lina mjadala mrefu duniani kote. 


Prof. Kitila amesisitiza kuwa tafiti zinaonesha kuwa mataifa yaliyoendelea kama Marekani na Ulaya yameingiza elimu ya ujasiriamali katika mitaala yao zaidi ya miaka kumi iliyopita na kuleta matokeo chanya katika kuongeza fursa za wahitimu kupata ajira, kujiajiri, kutoa michango katika usitawi wa jamii na kukuza uchumi.

Aidha, Prof Mkumbo wamewahakikishia mojawapo ya vipaumbele vya muhimu kabisa katika Wizara anayoiongoza ni kufanya kazi kwa nguvu zote ili kuhakikisha kwamba haiwakatishi tamaa vijana wenye mawazo ya ubunifu.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...