Mabibi Na Mabwana,
Kwa niaba ya familia ya marehemu Mzee Leonard Merere napenda kuchukua nafasi hii kuwataarifu kuwa kutakuwa na Misa na kuaga mwili wa mzee wetu siku ya jumamosi 02/21/09 saa 11 asubuhi, naambatanisha anuani ya sehemu ambayo misa itafayika hapo chini.
Tafadhalini mabibi na Mabwana tunaombwa kuzingatia muda na kufika kwa wakati ili kufanikisha shughuli ya kumuaga mzee pindi tupatapo ujumbe huu basi tuwataarifu wale wote watakaopenda kuhudhuria shughuli hii muhimu.
Jacob ,Naomi & Anna Merere wameniomba nisisahau kuwashukuru watu wote kwa ukarimu wao wa kuchangia kwa hali na mali kuhakikisha uwezekano wa kuupeleka mwili wa marehemu baba yao nyumbani Tanzania kwa mazishi.
HOSANA GOSPER CENTER,
120 Stafford st Worcester, MA
Contacts:Jacob & Anna Merere (978)-726-2227/(978)-957-2153
Naomi Merere (978)-413-3722/978)-632-9823
Juma Malika (781)-244-7353
Simon Twalipo (978)-423-1192
Pastor Abisalom Nasua (214)-554-7381

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Jacob na familia yote ya Merere, nawaombea mungu awabariki katika kipindi hiki kigumu.

    ReplyDelete
  2. Jamani natamani kuhudhuria hiyo misa ya kumuaga mzee mwenzangu lakini huo muda wa saa 11 asubuhi(hiyo ni alfajiri) sitaweza na uzee nilionao. Kama kutakuwa na mabadiliko ya muda msisite kunijulisha. Naweza kuhudhuria wakati wowote kuanzia saa 2 asubuhi.

    ReplyDelete
  3. Poleni sana Jacob na Naomi,Mungu awatie nguvu katika kipindi kigumu cha kumsindikiza Baba,Mungu ni Mwaminifu na roho mtakatifu awape faraja ya pekee.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...