Queen Suzy

MNENGUAJI mahiri nchini Queen Suzy usiku kuamkia leo katangazwa kujiengua rasmi kwenye bendi ya muziki wa dansi ya FM Academia na kurudi katika Kampuni aliyowahi kuitumikia ya African Stars Entertainment (ASET) ambapo amejiunga rasmi kuanzia sasa.


Utambulisho huo wa Queen Suzy ulifanyika kwenye ukumbi wa Club Bilicanas ambako bendi hiyo ilikuwa ikifanya onyesho lake la kila Jumatano linalofahamika kama ‘Out of Africa Nite’.


Mashabiki walipagawa na kutoamini kile walichokisikia na kukiona kutokana na dada huyo mrembo na mwenye machachari awapo jukwaani alipotambulishwa na kusakata sebene ipasavyo.


Akizungumza na Tanzania Daima mmoja wa wasemaji wa bendi ya Twanga Pepeta Abuu Semhando ‘Baba Diana’ alikiri kwamba Suzy amerudi kwenye Kampuni yake ya wali hivyo hilo siyo jambo geni.


“Ni kweli Suzy karudi nyumbani lakini kwa wale wasiomfahamu ama kujua historia yake watashangazwa lakini ikumbukwe kwamba ASET ndiyo Kampuni yake ya kwanza kumtambulisha kwenye jukwaa la kunengua na kupata jina kubwa” alisema Abuu.


Aidha Abuu aliwataja wacheza shoo wengine wawili kwa jina moja moja waliotambulishwa pamoja na Suzy Club Bilicanas kujiunga na Twanga Pepeta ni Asha na Sabrina.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. huyu karudi tu ili ajisogeze kwa kalala jr baba wa mtoto wake
    patamu hapo kwa huyo mary sijui itakuaje

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...