mwendeshaji wa kipindi kipya cha TV katika TBC1 Maria Shaba akiongea na mwakilishi toka ubalozi wa Uingereza nchini pamoja na prodyuza Dk. Martin Mhando na msanii Vitalis Maembe, Rose Haji wa MISA-Tan na Mh. John Mnyika wa CHADEMA baada ya kukamilisha kurekodi sehemu ya kwanza ya kipindi cha 'Kitimtim' kitachoanza kurushwa hivi karibunik ikiwa ni kuamsha na kuelimisha wananchi kuhusu wajibu na haki katika uchaguzi mkuu. Fungua dimba ni mada ya Ushiriki na utendaji wa vyombo vya habari katika uchaguzi mkuu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Nakupongeza Mama Maria Shaba,zidisha juhudi na maarifa zakutuelimisha kwani wengi wetu bado hatujui wajibu na haki za chaguzi zetu kitaifa
    Mpili

    ReplyDelete
  2. Ikiwezekana wakati wa kampeni ukifika mtuandalie mdahalo tujue wagombea urais watatufanyia nini na watafanyaje kufikia malengo hayo. Uchaguzi uliopita ulipita kimya kimya basi hata malengo ya rais hatukuyajua wala jinsi atakavyoyafikia. Lengo pekee lililokuwa wazi ni la kutengeneza ajira milioni moja. Haukutolewa ufafanuzi kwamba wanaohitaji ajira watakuwa wameongezeka kwa kiasi gani. Tumeambiwa malengo yametimia kwa kiasi kikubwa kupitia sekta isiyo rasmi lakini inakuwa vigumu kutofautisha walichokuwa wanakifanya kabla na ajira zao mpya.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...