Balozi wa Jamhuri ya Djibouti, Saidi Amin Shamo akielezea machache juu ya sherehe hiyo ambayo alikuwa ameiandaa nyumbani kwake. Kulia ni Mshereheshaji wa sherehe hiyo Baby Kabaye ambaye pia ni mtangazaji wa Choice Fm 102.6 FM.
Baadhi ya Wanachama wa Unity of Women Friends (UWF) wakiwa katika picha ya pamoja usiku huu nyumbani kwa balozi wa Djibout.
Pichani kati ni Mke wa Balozi wa Jamhuri ya Djibouti Bi. Mariam Shamo akiwa amepozi na wageni wake usiku huu,kushoto ni Prof. Faya mbaye ni mtaalamu wa magonjwa ya mifupa wa hospitali ya Aghakhan,jijini Dar pamoja na mwanae.

Mwanamuziki wa kimataifa ajulikanaye kwa jina la Ahmad Naji kutoka nchini Mogadishu akitumbuiza kwenye hafla hiyo usiku huu.
Mke wa Balozi wa Jamhuri ya Djibouti Bi. Mariam Shamo (katikati) akimtambulisha Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Clouds Media Group Bw. Joseph Kusaga (kushoto) kwa wageni waalikwa waliohudhuria katika hafla hiyo iliyofanyika nyumbani kwake usiku huu.
Balozi wa Marekani nchini Tanzania Bw. Alphonso E. Lenhardt (katikati) akimtambulisha mkewe kwa Balozi wa Uturuki Dk. Sander Gurbuz katika hafla iliyokuwa imeandaliwa na Balozi wa Djibout Bw. Shamo kwa ajili ya kumshukuru Mungu kufunga mwaka wa 2010 salama na kuukaribisha mwaka 2011. Pia ilihuhusu maadhimisho ya miaka 6 ya Universal TV yenye makao yake makuu nchini Uingereza.
Mke wa Balozi wa Jamhuri ya Djibouti Bi. Mariam Shamo akizungumza na Balozi wa Uturuki Dk. Sander Gurbuz aliyeambatana na mkewe katika hafla nyumbani waliyokuwa wameiandaa nyumbani kwao usiku huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Mithupu huyo mpiga gitaa anatoka nchi inayoitwa Mogadishu au Somalia? Maana kama bado nakumbuka mji mkuu wa Somalia ni Mogadishu. Sina hakika hiyo nchi ya Mogadishu ipo maeneo gani.

    ReplyDelete
  2. Mwaka haujaisha huu!
    Kumbe kuna NCHI inaitwa MOGADISHU!!
    Duh!

    ReplyDelete
  3. Hovyo! Mwandishi mzima? Eti nchi ya Mogadishu? Hovyo!

    ReplyDelete
  4. Naona Mwandishi anashambuliwa kwa kuwa eti ametaja kuwa kuna nchi ya "MOGADISHU", lakini mimi sijaona hilo jina Mogadishu kwenye habari hiyo, badala yake ninaona "JAMHURI YA DJIBOUTI". Hivi kuna matatizo ya uono na pengine usomaji kwa upande wangu au habari ilibadilika baadae?

    Mwenyeji wa Tanga- Ughaibuni

    ReplyDelete
  5. Absolutely positively Gorgeous Woman.I say this in a complimentary way

    ReplyDelete
  6. Bongo kweli wiki kadhaa mbele yaani mmeshamaliza mwaka? na party za kumaliza mwaka mmeshazila?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...