Mjomba aslaam aleikhu,
pole na kazi nyingi na salaam toka Njombe.

Jumamosi 12/03/2011 Laxmi Darts Club ya Tukuyu ilifanya ziara ya mchezo wa kirafiki mjini Njombe na kukutana na Club kongwe ya darts nchini iliyoanzishwa miaka ya 1950 – Kibena Club. Mchezo ulikutanisha kina mama na kina baba kwa pande zote mbili.

Wanyambala wa Tukuyu walionesha mchezo wa hali ya juu kwa kuwagalagaza wenyeji wao ambao wengi wao walikuwa raia wa kigeni kwa ushindi wa jumla wa mabao 15 kwa 3

Mchezaji Hendrick wa Kibena Club na Issa wa Laxmi ndiyo walikuwa nyota kwa pande zote mbili kwa kina baba na Mrs. Hendrick wa Kibena Club ndiye alikuwa nyota na mshindi wa Jumla kwa kina mama.

Hendrick wa Kibena akitoa ngoma kimiani


Mnyambala Issa wa Laxmi akitoa ngoma kimiani


Kibena ilibidi kuita majeshi ya akiba. Hapa Mzee mzima

akijaribu kuokoa jahazi isizame bila mafanikio.


Kina mama wakiwa ulingoni.... haikuwa kazi ndogo


Washindi wa pande zote mbili katika picha ya

pamoja wakisherehekea zawadi zao.


Moja ya mabango ndani ya Kibena Darts Club

yakionesha washindi wa miaka hiyooo ya 1950


Habari hii na picha na Mjomba Juma

wa Globu ya Jamii - Tukuyu



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...