Na Abdulaziz video
Zoezi la kufukua Maiti za watu
waliofunikwa na kifusi katika Machimbo ya Madini katika Kata ya Nandagala Wilayani
Ruangwa Mkoani Lindi jana limekamilika leo asubuhi ambapo maiti zote 7 zilipatikana.
Akiongea na Globu ya Jamii eneo la tukio, Diwani wa Kata hiyo, Bw. Andrew
Chikongwe alibainisha kuwa kazi ya kufukua kifusi hicho
imechukua muda mrefu kufuatia na kuwepo kwa zana duni za kufukua
Mchanga hali iliyofanya kazi hiyo kuwa Ngumu kuanzia jana saa 9 jioni hadi
leo asubuhi
Chikongwe aliwataja Marehemu hao ni Nyang'ana
Mkelecha,Mkazi wa Musoma, Mohamed Omari Fondogoro, Mkazi wa
Morogoro, Bakari Liganga mkazi wa Chunyu Ruangwa, Rajab maarufu ROGER Mkazi wa
Musoma, Uwesu Bakari Abeid mkazi wa Rondo, Chakoda Mkazi wa Dar na
Rashid Ally maarufu kama BADE Mkazi wa Masasi, mkoani Mtwara
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...