Itakumbukwa kuwa wakati wa Mkutano wa Nane wa Bunge uliofanyika kuanzia Juni - Agosti, 2012, Spika wa Bunge aliunda Kamati Ndogo ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge kuchunguza tuhuma zilizokuwepo kuwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini na baadhi ya Wabunge walijihusisha na Vitendo vya rushwa wakati wa mjadala wa Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini (2012/2013).
        Hivyo, Tangazo hili linatolewa kuuarifu Umma kwamba Kamati hiyo Ndogo imekamilisha kazi yake kama ilivyoelekezwa kwenye Hadidu za Rejea na kukabidhi Taarifa ya Uchunguzi huo kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano tarehe 27 Septemba, 2012.      
 Kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge (2007), Spika atatoa muongozo kuhusu utaratibu wa kufuata kuhusu uwasilishaji wa Taarifa hii Bungeni ambapo yaweza kuwa Spika akatoa uamuzi ama Kamati kuwasilisha Taaarifa hiyo Bungeni. 
       Spika atatoa taarifa ya kukamilika kwa uchunguzi huo Bungeni wakati wa Mkutano wa Tisa wa Bunge unaotarajia kuanza tarehe 30 Oktoba, 2012.      
       Hata hivyo baada ya Kamati hiyo kumaliza kazi yake baadhi ya wananchi, wanasiasa na vyombo vya habari vimeanza kuchambua na kuchapisha maudhui ya taarifa hiyo.  Kitendo cha kuchambua na kuchapisha maudhui ya taarifa hiyo katika vyombo vya habari ni kinyume cha sheria na kinaingilia uhuru, haki na madaraka ya Bunge kwa mujibu wa Kifungu cha 31(1)(g) cha Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge, SURA 296 (the Parliamentary Immunities, Powers and Privileges Act, CAP 296). 
Kifungu 31(1)…Any person who-
       (g) publishes, save by the general or special leave of      the Assembly, tiny paper report or other document    prepared expressly for submission to the Assembly           before the same has been laid on the Table  of the          Assembly;      
          ... shall be guilty of any offence and shall on conviction be liable to a fine not exceeding five hundred thousand shillings or to imprisonment for a term not exceeding three years or to both such fine and imprisonment. 
       Kifungu hiki kinakataza mtu yeyote kuchambua na kuchapisha taarifa ya Kamati kabla ya taarifa hiyo kuwasilishwa Bungeni. Ikithibitika kuwa taarifa hiyo imechahapishwa wahusika wanaweza kulipa faini isiyozidi shilingi laki tano au kifungo kisichozidi miaka mitatu au vyote. 
       Hivyo natoa rai kwa umma kuwa tuache Bunge lifanye kazi yake kwa mujibu wa Katiba, Sheria na Kanuni.     

Job Yustino Ndugai, (Mb.)
NAIBU SPIKA

25 Oktoba, 2012

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Kifungu hakikatazi chochote bali kinasema ukichapisha utakumbana na faini na/au kifungo. Kwa hiyo ni uamuzi wa mtu kuchapisha ama la.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...