Maonyesho ya 20 ya Siku ya Wakulima Tanzania (NaneNane) yameanza rasmi jana Agosti 1 katika viwanja vya Nzuguni mjini Dodoma.Maonyesho hayo ambayo yapo chini ya Udhamini Mkubwa wa TIB Development Bank,yanaendelea kwa kasi mpaka hapo itakapofikia kilele chake Agosti 8,2013.
Sehemu ya Ngoma za asili zikiendelea kutumbuiza katika ugunguzi wa Maonyesho hayo ya 20 ya Siku ya Wakulima Tanzania (NaneNane) yanayoendelea kwenye viwanja Nzuguni mjini Dodoma.
Baadhi ya Wageni na Viongozi wakifatilia Burudani hiyo ya ngoma.
Muonekano wa Jengo la Mdhamini Mkuu wa Maonyesho hayo mwaka huu wa 2013.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Kwa hiyo siku hizi haiitwi tena TIB(TANZANIA DEVPT BANK)? Bali TIB DEVPT BANK LTD......oooh kumbe!

    ReplyDelete
  2. Duuuh haya majina ebu tuwe tunayaweka inavostahili maana hata inakuwa haieleweki tunamaanisha nini. Badala ya kumtangaza mdhamini wako unakuwa unamdhalilisha. Nao wadhamini wanatakiwa wahakiki mabanko yanayoenda kwa jamii kabla ya kuwekwa. Inawezekana ni mie tu naona huo mkanganyiko wa jina la hiyo benki.

    ReplyDelete
  3. Mdau, Benki ya Rasilimali Tanzania (Tanzania Investment Bank) imebadili jina na sasa inajulikana kama Benki ya Maendeleo ya TIB (TIB Development Bank).

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...