Mkuu
wa mkoa wa Mtwara Mhe Joseph Simbakalia akimkaribisha Waziri wa Nishati na
Madini pamoja na ujumbe alioambatana nao akiwemo balozi wa China nchini Bw….
Mara baada ya kufika ofisini kwake kuelezea uwepo wapo katika mkoa huo
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe John Simbakalia akimweleza Waziri wa
Nishati na Madini jambo linalohusu sekta ya umeme ambapo Prof. Muhongo
anaisimamia ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Mkandarasi
anayehusika na usambazaji wa umeme vijijini Bwana Luta (mwenye shati nyeupe), mara baada ya kusimamishwa na Waziri wa Nishati na Madini
Prof Muhongo ili kuelezea maendeleo aliyoyafikia katika kukamilisha mradi huo
kulia kwake ni Mkurugenziwa Huduma za Ufundi (REA) Injinia Bengiel H. Msofe.
Prof
Muhongo na balozi wa China wakikgua mtambo wa kuchujia maji uliopo katika
maeneo ya makazi ya watumishi ambao utawasaidia wananchi wanaozunguka eneo hilo
kupata huduma ya maji safi na salama.
Waziri wa Nishati na Madini na ujumbe wake wakikagua mradi wa ujenzi wa nyumba za kuishi watumishi wa mtambo wa kufua gesi lililopo katika eneo la Madimba Mkoani Mtwara
Baadhi ya nyumba zitakazotumika kwa kuishi
watumishi wa eneo la kuchakata gesi Madimba ni nyumba za kisasa zilizojegwa kwa
ubora mkubwa sana kama zinavyoonekana.
--------------------------
Waziri
wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo akiambatana na Balozi wa China
nchini Dk. Lu Youging wamefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa bomba
la gesi linalotarajiwa kuleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi kwa watanzania na
hivyo kuchangia kuiingiza nchi kati ya nchi zenye uchumi wa kati ifikapo 2025.
Akizungumza
na waandishi wa habari balozi alisema ziara za kukagua bomba la gesi zinalenga
katika kuhakikisha kazi inayofanyika ni bora na ipo katika viwango
vinavyotakiwa na kuifanya nchi yake kuwa sehemu ya mradi na maendeleo ya nchi.
Kwa
upande wake Prof. Muhongo amefurahishwa na maendeleo ya ujenzi wa mradi huo na
kukiri kuwa kila mara afanyapo ziara kwenye miradi hiyo anakuta mabadiliko
makubwa yanayomfanya kufurahia juhudi ya wakandarasi itakayopelekea mradi
kukamilika kwa wakati uliopagwa mezi desemba 2014.
“Jamani
ni nani walikuwepo tulipokuwa tukikabidhiwa eneo hili kwa ajili ya kuanza
mradi? Eneo hili lilijaa mikorosho tu, lakini sasa tunaona kazi kubwa ya ujenzi
iliyofanywa na wakandarasi hawa.
Aidha
Muhongo alipotakiwa kueleza manufaa watakayoyapata wananchi wa Lindi na Mtwara
alishangaa kuona kuwa bado watu hawaoni manufaa hayo na kuwaeleza waandishi wa
habari kutosubiri yeye ndio aseme wakati wao wenyewe wanashuhudia wananchi
wakipata ajira, huduma za jamii zikiboreka, wakipewa kipaumbele katika masuala
ya elimu.
Hata
hivyo Muhongo amewaeleza wanamtwara kuwa wasitegemee manufaa ya kuwepo kwa
rasilimali ya gesi ni kuwagawia pesa aidha wanatakiwa kujiendeleza kielimu na
kutumia fursa zinazojitokeza ikiwa ni pamoja na ufadhili wa masomo vilivyo ili
waweze kujikwamua kimaisha na kushiriki katika kunufaika na gesi iliyogunduliwa
katika eneo lao.
Akizungumzia
suala la kukamilika kwa mradi huo msimamizi wa ujenzi wa bomba hilo Injinia
Balthazar Mrosso alisema limekamilika kwa asilimia 70 na maeneo yaliyosalia ni
yale yanayohitaji umakini mkubwa ikiwa ni pamoja na maeneo yanayoathiriwa na
mafuriko pembezoni mwa mto wa Ruvu ambako kazi ya kuchimba mashimo ili kufukia
mabomba hayo inaendelea, maeneo yenye miinuko na madaraja.
Akielezea
suala la kukamilika kwa miradi ya kusambaza umeme vijijini Prof. Muhongo
amesema miradi yote nchini inatakiwa kukamilika ifikapo juni 2015 na kuagiza
mkandarasi asiye na uwezo wa kufanya hivyo kurudisha mradi huo apewe mtu mwenye
uwezo.
Muhongo
alimtaka mkandarasi Luta kuelezea hatua aliyofikia katika kusambaza umeme huo
katika mkoa wa Mtwara ambapo alieleza kuwa suala la kusafisha mkuza
limekamilika pamoja na kusambazwa na kusimikwa kwa nguzo kwa eneo Fulani. Aidha
Mkandarasi Luta alimhakikishia Profesa Muhongo kuwa mradi huo utakamilika kwa
wakati.
Akitanabaisha
nia ya dhati ya kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati Muhongo alisema
kuanzia mwezi huu hadi mwezi Oktoba atakagua miradi yote ya REA II na kwa
wakandarasi watakaoonesha kutoridhisha kupokonywa miradi. “Hatutasubiri kufika
mwezi juni ndipo tuanze kufukuzana na kukamilika kwa miradi mpaka desemba
wakandarasi watakaoonesha kuzubaa watapokonywa na kupewa mtu mwingine awe mzawa
au mgeni” alisisitiza Muhongo.
Tangia
kuanza kutekelezwa kwa mradi huo mkubwa wa Bomba la gesi hii ni mara ya tatu
kwa profesa Muhongo kuzungukia maeneo hayo kujionea jinsi kazi inavyofanyika na
kukiri kufurahishwa na kasi ya wakandarasi hao.
Serikali kupitia mkuu wa mkoa wa Mtwara inabidi kuanza kupromote mkoa huu.inabidi mkae kibiashara zaidi, trust me zaidi ya Gas na Kiwanda cha Saruji ambavyo vinajitangaza vyenyewe hakuna effort yoyote on the side of the Government kupromote eneo hili..
ReplyDeleteMkimaliza miaka 10 muuziane kama Oysterbay
ReplyDelete