Na
Athumani Shariff (MoW)
Waziri wa Maji Prof. Jumanne Maghembe, leo
amezindua rasmi BODI mpya ya Shirika la majisafi na Usafi wa Mazingira
(DAWASCO) inayoundwa na wajumbe 13. BODI hii imeundwa baada ya ile ya zamani kumaliza muda
wake.
Bodi hiyo mpya imeteuliwa tangu tarehe
1/8/2014 inayojumuisha wataalam mbalimbali wakiwemo maprofesa wa chuo kikuu cha
Dar es Salaam, viongozi wa kisiasa na asasi za kiraia inaongozwa na Mwenyekiti
Meja Generali Mstaafu Samweli Kitundu.
Pia wamo Nehemia Mchechu, Mkurugenzi
Mtendaji Shirika la Nyumba la Taifa, Prof. Samweli Maghimbi Chuo Kikuu cha Dar
es Salaam, Dkt. Marcelina Chijiriga Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Teresia
Mbando katibu Tawala Ofisi ya Mku wa Mkoa wa Dar es Salaam, Hawa Sinare Mwenyekiti
wa BODI ya DAWASA.
Wengine ni Inj. Ray Seng’enge, Abubakari
Kunenge, Inj. Boniface Muhegi, Iddi Azan Zungu, Blangson Hamisi na Katibu wao
Jackson Midala Mkurugenzi wa Shirika la Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es
Salaam (DAWASCO).
Profesa Maghembe aliitaka BODI hiyo
kuzikabili vilivyo changamoto zote zinazolikabili shirika hilo, hususan upotevu
wa maji ambao umefikia asilimia 55 sasa.
“Naagiza muunde mara moja kitengo cha
ki-intelijensia zaidi kitakachoripoti mara moja kwenye bodi yenu juu ya wizi wa
maji” Aliagiza Waziri Maghembe.
Waziri alisema, hivi karibuni tunategemea
kupata maji mengi sana kwa ajili ya jiji la Dar es Salaam, hivyo yatakuwa
hayana umuhimu endapo yakuwa yanapotea wakati serikali imeekeza pesa nyingi
sana katika kuyaleta. Alieleza Waziri Maghembe.
Pia aliitaka BODI iandae mpango wa kulipa
madeni yanayodaiwa haswa na shirika la umeme Tanzania (TANESCO) ili kuepuka
kusitishiwa huduma hiyo.
Katika hatua nyingine Waziri Maghembe
aliitaka BODI hiyo ifanye marekebisho ya menejimenti ili kuleta ufanisi zaidi
wa kazi.
Mwisho aliwaambia wafanye kazi kwa bidii
wakizingatia matokeo, na aliwaambia kuwa Wizara ya Maji inatekeleza mipango
yake kwa haraka kwa utaratibu wa TEKELEZA SASA KWA MATOKEO MAKUBWA yaani BIG
RESULTS NOW hivyo ni lazima wajiunge na familia ya maji kwa kufanya kazi kwa
utaratibu huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...