Na Sultani Kipingo, Mahakamani
UPANDE wa Jamhuri katika kesi inayomkabili aliyekuwa  Mkurugenzi wa Mlamkala ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Ephraimu Mgawe na msaidizi wake, umedai kwamba upelelezi umekamilika dhidi ya tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka kwa kusaini mkataba wa kuipa kazi Kampuni ya Ujenzi ya China Communications Ltd bila kutangaza zabuni.
Madai hayo yalitolewa leo na upande wa Jamhuri katika kesi hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Mfawidhi, Isaya Arufani kwamba upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.
Mbali na Mgawe mshtakiwa mwingine ni, Naibu Mkurugenzi Mkuu PTA, Hamadi Koshuma.
Upande wa Jamhuri uliongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Osward Tibabyekomya  akisaidiana na Mwendesha  Mashitaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Ben Linkolin.
“Mheshimiwa hakimu upelelezi wa kesi hii umekamilika upande wa Jamhuri tunaomba tarehe ya kusikiliza maelezo ya awali…” alidia mheshimiwa Linkolin.
Hakimu Arufani alisema mahakama hiyo itasikiliza maelezo ya awali Septemba 11, mwaka huu na dhamana ya washtakiwa inaendelea.
Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa kuwa Desemba 5, mwaka 2011 huko TPA, washtakiwa wakiwa waajiriwa wa mamlaka hiyo kwa nyadhifa hizo, walitumia vibaya madaraka yao.
Ilidaiwa kuwa washtakiwa walitumia vibaya madaraka yao baada ya kusaini mkataba kati ya TPA na Kampuni ya China Communications na kuipa kazi ya ujenzi wa geti namba 13 na 14 la mamlaka hyo, bila kutangaza zabuni  kinyume cha kifungu cha 31 cha sheria ya manunuzi namba 21 ya mwaka 2004. 
Washtakiwa walikana mashitaka yao kwa nyakati tofauti.
Mapema Agosti 23, mwaka 2012 jijini Dar es Salaam, Waziri wa Uchukuzi Dk. Harisson Mwakyembe, alimsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu, Ephrahim Mgawe pamoja na wasaidizi wake wawili ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazowakabili.
Wengine waliosimamishwa ni Meneja wa Mafuta ya Ndege Kurasini, Meneja wa JET na Meneja wa Oil Terminal kutokana na tuhuma za kupotea kwa mafuta na kuidanganya serikali kuhusu mafuta masafi na machafu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...