KOCHA wa Yanga, Mbrazil Marcio Maximo amewaaga rasmi leo asubuhi wachezaji wa timu hiyo kwenye mazoezi uwanja wa Sekondari ya Loyola huku akitarajia kuvuna zaidi ya Milioni 20 ndani ya klabu hiyo ikiwa ni mshahara wake wa dola 1200 na yupo kwenye harakati za kudai fidia ya kuvunjiwa mkataba na kuletwa mrithi wake kabla uongozi wa klabu hiyo haujamaliza nae.
Hata hivyo, tayari Maximo ameaga wachezaji wake kwenye mazoezi ya asubuhi leo ambapo mazoezi hayo yaligeuka shubiri baada ya Maximo kuwakusanya wachezaji wake na kuwambia kuwa kuanzia leo sio kocha wa timu hiyo tena na kuwatakia maisha mema ndani ya klabu hiyo ya Jangwani.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wachezaji wa klabu hiyo ambao pia hawajaridhishwa na uamuzi wa uongozi wa klabu hiyo kumuacha mshambuliaji Hamis Kiiza na kumsajili Amis Tambwe.
Mmoja wa wachezaji hao alisema "Ni kweli kocha ametuaga asubuhi daa! ndio hivyo tumesikitika lakini hatuna jinsi."
Naye mchezaji mwingine ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema "Inaumiza sana jana (juzi) tumefanya nae mazoezi vizuri kabisa tena amechangamka kama kawaida kumbe nyuma kuna mambo yanaendelea, leo asubuhi tumeenda mazoezi kama kawaida tukijua tunafanya mazoezi matokeo yake anasema acheni kila kitu kaeni hapo nataka kuzungumza na nyinyi.
Mnyama nomah.... !!! Hata aje Morinho dozi ipo pale pale...
ReplyDeleteWaache unafiki wanalia nini wakati wao ndo waliomponza kwa kucheza chini ya kiwango. Wana bahati kwamba Yanga ya sasa sio kama ile ya Enzi zile vinginevyo wangekula bakora wote haiwezekani kila mechi na Simba wachezaji wanafanya madudu.
ReplyDeleteTunampenda, lakini kama hana msaada kwa timu aende tu. Na uongozi sijui kwa nini wanang'ang'ania kuwasajili wachezaji wa Simba! Angalia matatizo tuliyopata kwa Okwi na Kaseja! Wajaribu kuwa wanasajili wachezaji wenye mapenzi na timu, sio tu bora katoka Simba!
ReplyDelete