Kwa masikitiko makubwa klabu ya Simba inawaarifu umma kupitia vyombo vya habari.uamuzi wake wa kuvunja mikataba yake na makocha wake  - kocha mkuu Dylan Kerr kutoka uingereza na kocha wake wa makipa Iddi Salim.
Katika uamuzi wake uliofanywa mchana huu na kikao cha kamati ya utendaji, ambapo makocha hao waliitwa, klabu ya Simba na walimu hao kwa pamoja wamekubaliana kuvunja mikataba ya ajira zao kwa faida ya pande zote mbili.
Kwa sasa kocha msaidizi wa Simba Jackson Mayanja atakuwa na timu.huku mchakato wa kumpata kocha mkuu ukiendelea.
Mwisho uongozi unawashukuru walimu hao kwa huduma waliyoitoa katika kipindi chote cha uwepo wao klabuni.

Imetolewa na Haji S.Manara
Mkuu wa mawasiliano wa klabu ya Simba.
Simba nguvu moja

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...