Mkuu wa Shule amewapongeza sana Wanafunzi waliohitimu kidato cha nne mwaka 2015 na kwa Ufaulu mzuri. Pia amewamwagia sifa kemkem Walimu kwa ujumla huku akipongeza Wazazi, uongozi wa shule hiyo kwa kufanikisha siku hii ya leo kwa kumshukuru Mungu kwani amejibu Sala zao na kuwawezesha wote kufaulu vizuri mtihani wao wa Taifa. Mwaka 2015 Wanafunzi 47 walisajiliwa kufanya Mtihani wa Taifa kidato cha Nne, Wanafunzi 36 wamefaulu kwa Daraja la kwanza na Wanafunzi 11 wamefaulu kwa daraja la pili. Katika matokeo haya Shule imekuwa ya 2 kati ya shule 192 Kimkoa na ya 17 kati ya Shule 3452 Kitaifa. Aidha , wanampongeza Mkuu wa Shule, Mkurugenzi na Uongozi mzima kwa uwezeshaji mkubwa sana hadi kufikia mafanikio hayo.
Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Magharibi-Bukoba Abedinego Kesho mshahara ndiye aliyeongoza Ibada Shuleni hapo leo.
Wanafunzi wakiimba Wimbo wa Kwaya ya RC Josiah SS wakati wa Ibada ya Shukrani leo hii jumamosi
Wanafunzi wa Josiah wakifuatilia kwa karibu Ibada hiyo
Mwenyekiti wa bodi ya shule, Johansen Rutabingwa akiongea wakati wa Ibada hiyo.  Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...