Katika kudumisha urafiki
mwema kati ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete katika
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (JKCI) na Hospitali ya Moyo ya Wolfson iliyoko jijini Tel Aviv, Israel, Kaimu Mkurugenzi wa
JKCI Profesa Mohamed Janabi amefanya
ziara kutembelea hospitali hiyo na kuonana na madaktari bingwa wa moyo pamoja
na watoto wa Kitanzania kadhaa waliopewa rufaa kwenda kupata matibabu hapo.
Profesa Janabi ameiambia
Globu ya Jamii kwa njia ya simu kutoka Tel Aviv kuwa Serikali ya Israel kupitia
mpango wake wa Save a Child's Heart (Okoa moyo wa mtoto) ni moja ya washirika
wakubwa wa JKCA katika kubadilishana utaalamu na vifaa.
“Washirika wetu wengine ni Open Heart
international ya Australia, Mending Kids Heart ya California, Madaktari Africa ya South
Carolina, Almutada ya Saudi Arabia, Sharjah International ya UAE na Madras Medical
mission and BLK ya India.
“Hawa wote kwa muda mbalimbali
huw wanakuja JKCI na mpaka sasa katika
mwaka huu wa 2016 wamekuja BLK, Madaktari Africa na lsrael” alisema, na
kuongezea kuwa “Kwenye hospital ya moyo ya Wolfson tunayoshirikiana nayo JKCI.
Nimeona watoto wetu 11 tuliowaleta huku wakiwa na complicated cases. Tisa
wamekwisha fanyiwa upasuaji bado wawili na wote wanatokea Zanzibar.
Profesa Janabi ameongozana
na manesi watatu na daktari mmoja.
Kaimu Mkurugenzi wa JKCI Profesa Mohamed Janabi baadhi ya wenyeji wake katika Hospitali ya Moyo ya Wolfson iliyoko jijini Tel Aviv, Israel, wakati wa ziara yake
Kaimu Mkurugenzi wa JKCI Profesa Mohamed Janabi akiwa na madaktari bingwa wa moyo katika Hospitali ya Moyo ya Wolfson iliyoko jijini Tel Aviv, Israel, wakati wa ziara yake
Kaimu Mkurugenzi wa JKCI Profesa Mohamed Janabi akiongea na Mkuu wa Hospitali ya Moyo ya Wolfson iliyoko jijini Tel Aviv, Israel, wakati wa ziara yake
Kaimu Mkurugenzi wa JKCI Profesa Mohamed Janabi akiwa ametoka kusaidia upasuaji na madaktari bingwa wa moyo katika Hospitali ya Moyo ya Wolfson iliyoko jijini Tel Aviv, Israel, wakati wa ziara yake
Kaimu Mkurugenzi wa JKCI Profesa Mohamed Janabi akiwa na baadhi ya wagonjwa na walezi wao waliofanyiwa upasuaji katika Hospitali ya Moyo ya Wolfson iliyoko jijini Tel Aviv, Israel, wakati wa ziara yake. Bango aliloshika linaonesha majina ya wagonjwa kutoka Tanzania waliofanyiwa upasuaji
Mungu akubariki kwenye majukumu yako profesa. unaonekana wazi ni mtu muhimu sana
ReplyDelete