Na  Bashir  Yakub.  

Kazi  kubwa  ya  sheria  zote  zinazoshughulika  na  masuala   ya  ardhi   ni kuratibu  na  kutoa  mwongozo  katika   miamala  mbalimbali  ya masuala ya ardhi  katika  maisha  ya  kila  siku. 

Miamala  hiyo  ni  kama  uuzaji  na  ununuzi  wa  ardhi, masuala  ya  mikopo  na  rehani, upangaji  na  upangishaji, masuala  ya  fidia, kuhamisha  umiliki, haki  na  wajibu wa  mmiliki ardhi, haki  na  wajibu  wa  serikali  katika  ardhi  yote, upimaji  na  ramani, namna ya kutatua  migogoro  ya  ardhi, n.k. 

Makala  yatagusa  kwa  mtindo  wa  dondoo  baadhi  ya  mambo  ya  msingi  yaliyo  katika  sheria  ya ardhi namba  4 ya  1999  sura  ya  113.

1.SHERIA  NAMBA  4  YA MWAKA 1999.

Sheria  hii  ilipitishwa  na  bunge  la  Jamhuri  ya  Muungano  mwaka 1999.  Hata  hivyo  ilianza  kutumika  rasmi  mwezi  mei  mwaka  2001.

( a ) MDHAMINI  WA  ARDHI  YOTE NI  RAIS. 

Sehemu  ya  pili  ya  kifungu  cha  3  cha  sheria  hii  inaanza  kwa  kueleza  sera  ya  taifa  ya  ardhi. Kubwa  linalotajwa  ni  kuwa  ardhi  yote  ni  mali  ya  umma  ambayo  mdhamini  wake    ni  rais  wa  Jamhuri  ya  Muuungano  wa  Tanzania. Huu  ndio  msingi  mkuu  wa  ardhi  yetu.

( b ) WASIMAMIZI   WAKUU   WA  ARDHI.

Sehemu  ya  iv  kifungu  cha  8  mpaka  18  kinaeleza   watumishi  wakuu  na  wasimamizi  wa  ardhi  kitaifa. Waziri  wa  ardhi  ndiye  mwenye  dhamana  kuu  akifuatiwa  na  kamishna  mkuu  wa  ardhi  kabla  ya   kutajwa  kamishna  msaidizi  na  baadae maafisa  ardhi . Wajibu,  kazi  na  majukumu  yao  yameainishwa  katika  vifungu  hivyo. Sambamba  na  hilo  mipaka  katika  utekelezaji  wa  majukumu  yao  ni  jambo  jingine lililoainishwa.

( c ) KUMILIKI   HATI.

Sehemu  ya vi  kifungu  cha  24 mpaka  30  yameelezwa  masuala  ya  hakimiliki.  Taratibu  za  kupata  hakimiliki  na  umilikishwaji .  Wakati  huohuo  vifungu  vya 31  mpaka  35  vimeeleza  vyema  masharti  yanayoambatana    na  hakimiliki ,muda  wa  hakimiliki  pamoja  na  kodi  za ardhi.

Kifungu  cha  76  mpaka  78  kimeongelea  uuzaji  wa  ardhi   hasa  zenye  hati miliki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...