Madaktari wa Tanzania katika hospitali ya taifa ya Muhimbili, Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, wakishirikiana na wenzao wa India wamefanikiwa kufanya upasuaji wa moyo wa aina yake Tanzania.
Upasuaji huo ujulikanao kama ‘bypass surgery’ ulishirikisha kupandikizwa kwa mishipa ya damu kutoka sehemu nyingine ya mwili moyoni bila kutumia mashine ya kusimamisha moyo na mapafu.
Kwa kawaida madaktari wanasema upasuaji wa moyo hufanyika baada ya moyo na mapafu kusimama, lakini upasuaji huo ulifanyika wakati moyo na mapafu vikifanya kazi.
Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa Dkt. Bashir Nyangasa ameambia BBC kuwa upasuaji huo wa kupandikiza mishipa ya damu nje ya mshine ni wa kihistoria nchini Tanzania.
Tunawapongeza madaktari wetu. Waandishi wa Tanzania ni wa ajabu. Tukio kama hili wameshindwa kulipa kipaumbele. Wao wamekalia siasa na kuandika mambo yasiyokuwa na tija. Tujivunie mafanikio yetu na kuyatangaza. Hongereni sana madaktari.
ReplyDeleteTuendelea kuimarisha huduma za afya nchini.
ReplyDelete