Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Francis Miti.


Na Woinde Shizza,Monduli

Imeelezwa kuwa Asilimia 10 ya watoto wilayani Monduli wanatajwa kutokwenda shule kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo utoro,pamoja na kufanya biashara katika baadhi ya minada wilayani humo jambo ambalo limeamsha hisia za viongozi wa wilaya na kuamua kufanya operesheni ya kuwakamata na kuwapeleka shule kwa lazima Zaidi ya watoto 21.

Hayo yameelezwa leo naAfisa elimu msingi Theresia Kyala kutoka wilaya ya Monduli mara baada ya ya zoezi la ukamataji wa watoto watoro amnao wanafanya biashara eneo la minada ambapo zoezi hilo lilifanyika mnada wa katika eneo la losirwa iliyoko kata ya mto wa mbu iko ambapo ni utekelezaji wa agizo la Mkuu wa wilaya ya Monduli bw,Francis Miti ambapo eneo hilo lina wakazi laki tatu kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012 huku Zaidi wakiwa ni wakazi wa jamii ya kifugaji.

Ambapo zoezi hilo limeendeshwa chininya usisamizi wa mkuu huyo na uongozi wa idara ya elimu imetembelea eneo la mnada wa Kigongoni na kuona watoto namna ambavyo wanaendelea kufanya biashara ndani ya mnada huo wakati wenzao wakiwa madarasani ambapo nikazungumza na baadhi ya watoto hao ambao wanaelezea baadhi ya sababu zilizowapelekea kutokwenda shule ikiwemo ugumu wa maisha huku wengine wakishindwa kujielezea.

Theresia Kyara ni afisa elimu msingi wilayani Monduli alisema kuwazoezi la operesheni hiyo wameianza rasmi katika soko la Alhamisi la eneo la monduli mjini na kufanikiwa kukamata watoto 16 na leo hii wamekamata watoto 21 hii kati ya hao watoto sita wamepelekwa bweni shule ya Manyara inaongeza idadi ya watoto ambao hawajaenda shule katika wilaya hiyo.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya hiyo ya Monduli Francis Miti amesema kuwa ameamua kutoa agizo hilo na kutekelezwa kwa lengo la kuwawezesha kwa kila mtoto mwenye sifa ya kwenda shule aweze kupata elimu hiyo ya kuanzaia msingi bure kwa lengo la kumuunga mkono mh,Rais katika utoaji wa elimu bure ili kuweza kuweza kushinda katika sekta ya elimu.

Pia amewataka wazazi wote wenye watoto kuhakikisha wanapeleka shule watoto wao na kuwaandikisha na endapo mzazi ama mlezi atakae mhusisha na kumkataza mtoto wake hatua za kisheria zitachukuliwa.Mkuu wa wilaya ya Monduli ameongeza kuwa zoezi hili la ukamatwaji wa watoto hao ambao kati yao wapo waliotoka kwaajili ya kuchunga katika minada huku wengine wakiwa hawajasoma kabisaa.

Nae mmoja wa mzazi bi,Moses ole laizer amesema kuwa zoezi hilo la kukamata watoto hao litaleta tija katika jamii kutokana na kuwa hakuna sababu inayofanya watoto hao wasiende shule kutokana na elimu kuwa bure na wazazi kuwaachia baadhi yao kuenda kufanya biashara minadani.Aliongeza kuwa baadhi ya Jamii za kifugaji hususani wamasai wamekuwa na muamko mdogo wa kupeleka watoto wao kupata elimu jambo ambalo linawanyima haki ya msingi kwa kila mtoto mwenye sifa kwenda shule

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...