Na Rabi Hume, Modewjiblog.

Katika kusaidia kukamilika kwa Mpango wa Maendeleo Endelevu ambao unataraji kumalizika 2030, Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF) imefanya warsha ambayo imekutanisha wadau mbalimbali ili kuona ni jinsi gani wanaweza kubadilishana mawazo ili kufanikisha mpango huo nchini.

Mgeni rasmi katika warsha hiyo alikuwa ni Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na Kuinua Uchumi kutoka Wizara ya Fedha, Anna Mwasha ambaye wakati akifungua warsha hiyo alisema kuwa mpango huo ni muhiu wa nchi yetu kwa sababu unakwenda kubadili maisha ya kila Mtanzania ili kuondokana na umaskini na kuwa katika maisha bora kama jinsi malengo 17 ya mpango huo yanavyojieleza.

Mo Dewji Blog ilipata nafasi ya kuhudhuria mkutano huo na kukuandalia habaroi picha jinsi warsha hivyo ilivyofanyika katika ukumbi wa ESRF.
DSC_2311
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida akitoa neno la ufunguzi katika warsa iliyoandaliwa na ESRF ili kuzungumzia Mpango wa Mendeleo Endelevu (SDG). (Picha zote na Rabi Hume, Modewjiblog)
DSC_2330
Baadhi ya washiriki waliohudhuria warsha hiyo wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii, Dkt. Tausi Kida wakati akifungua warsha hiyo.
DSC_2341
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Awa Dabo akitoa neno kwa niaba ya UNDP ambao ndiyo wasimamizi wa mpango huo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida na Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na Kuinua Uchumi kutoka Wizara ya Fedha, Anna Mwasha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...