Wajumbe wa Mkutano wa Majaji Wanawake Duniani kutoka Mahakama ya Tanzania wakiwa katika ufunguzi wa mkutano huo Washington DC Marekani. Mkutano huo unawakutanisha Majaji na Mahakimu kutoka nchi 92 Duniani kuwezesha kujadili pamoja na mambo mengine wajibu wao katika kuhakikisha kuwa wanatenda haki wanapotekeleza majukumu yao. Ujumbe wa Tanzania una jumla ya wawakilishi 53.
Ujumbe wa Mahakama ukionekana kwa mbali ukiwa katika ufunguzi rasmi wa Mkutano huo wa Wahe. Majaji Wanawake duniani.
Baadhi ya Majaji, Mahakimu na Viongozi wawakilishi wa Mahakama ya Tanzania katika picha ya pamoja nchini Marekani.
Baadhi ya Wajumbe kutoka Mahakama ya Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi pindi walipotembelea Ubalozi wa Tanzania nchini humo, Balozi Masilingi amefurahishwa na ugeni huo nao ujumbe wa Mahakama umesifu mapokezi mazuri yaliyotolewa na ubalozi huo toka walipofika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...