Bonanza maalum kwa ajili ya wanavyuo wa vyuo vya elimu ya juu mkoani Arusha lililofanyika mwishoni mwa wiki (Mei 21, 2016) Jijini Arusha lilifana, huku idadi kubwa ya wanafunzi wakijiunga na Mpango wa Uchangiaji wa Hiari wa PSPF.

Viongozi wa vyuo mbalimbali mkoani wakiwa katika picha ya pamoja Afisa Mfawidhi wa PSPF Arusha Bw. Philbert Leina (wa tatu kutoka kushoto, mstari wa nyuma)  baada kikao cha maandalii kilicho fanyika katika ofisi za PSPF mkoa wa Arusha.

Tamasha hilo lililofanyika katika viwanja vya chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kilichopo Njiro jijini Arusha, lilijumuisha vyuo vya Makumira, Mt. Meru, SAUT, MAN U (Chuo Kikuu cha Arusha), Chuo cha Ufundi Arusha na IAA.
Wanachuo wa IAA, wakishangilia baada ya timu yao kuibuka mshindi katika mpira wa miguu.

Michezo iliyoshindaniwa ni pamoja na Football, Netball, Basketball na Volleyball, hata hivyo mchezo uliovuta hisia za washiriki wengi ni mchezo wa mpira wa miguu ambapo timu ya Chuo cha Uhasibu Arusha kilibuka mshindi
Wanachuo wakifatilia Burudani kutoka kwa Mjomba Band
Akifungua mashindano hayo, Katibu tawala wa mkoa wa Arusha Bw. Daniel Machunda aliwataka wanavyuo hao kutumia michezo hiyo kama sehemu ya kujenga uhusiano Mwema na ushirikianao kati ya vyuo na kati ya yao wenyewe.

Pia aliishukuru PSPF kwa kuandaa Bonanza hilo ambalo msingi wake mkubwa ulikuwa ni kuwaelimisha wanavyuo juu ya huduma za PSPF. “Hili jambo mnalofanya PSPF ni jambo zuri sana kwa wanafunzi wa vyuo vya Arusha pamoja kutoa burudani lakini pia mnawapatia ufahamu juu ya Mfuko wenu (PSPF), hili ni jambo zuri sana na ninawaomba wana vyuo kuazingatia elimu mtakayopatiwa na wakati ukifika mfanye maamuzi sahihi,” alisema Bw. Machunda.
Ukaguzi wa timu kabla ya mchezo, wa tatu kulia ni Afisa Mfawidhi wa PSPF Arusha Bw. Philbert Leina.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...