Na Woinde Shizza,Arusha

Timu ya Intersport club yaibuka kidedea katika Tamasha la vijana mara baada ya kuifunga Club ya mairiva bao 3 kwa 1 katika fainali iliyofanyika katika uwanja wa Shekhe Amir Abeid uliopo Jijini Arusha.

Tamsha hilo ambalo lilianza mapema mwanzoni mwa mwezi huu limeweza kufikia tamati huku vijana wakiwatoa wito kwa wadau mbalimbali wa michezo kujitokeza kuanzisha mashindano kama haya kwani yanawasiadia kwa kiasi kikubwa

Akizungumza wakati wa fainali za mashindano hayo muuandaaji wa mashindano hayo ambaye ni mwenyekiti wa CCM kata ya Sakina Neema Mollel alisema kuwa lengo la kuanzisha tamasha hili la vijana ni kuwaleta pamoja vijana na kuwapa elimu ya jinsi ya kupiga vita utumiaji wa madawa ya kulevya kwa vijana

Alisema kuwa vijana wengi wamekuwa wanajishirikisha na utumiaaji wa madawa ya kulevya ivyo aliona ni bora akatumia muda huu kuwaleta pamoja ili kuwapa elimu pamoja na kuwashirikisha katika tamasha hili la michezo ambalo limeweza kuwafundisha vijana wengi huku wengine wakiwa wameamua kuaachana kabisa na kutumia madawa haya ya kulevya badala yake wameamua kushiriki katika mazoezi pamoja na michezo

"nia alisi ya kuandaa mashindano haya ni kuwaleta kwa pamoja vijana pamoja na kupiga vita madawa ya kulevya kwa vijana,kuwaleta vijana pamoja,kuwaondoa vijana wasiendelee kukaa mitaani bila kazi kwani michezo ni ajira"Alisema Neema Mollel

Aidha aliwataka wazazi na jamii kwa ujumla kuwajengea vijana misingi Imara ilikuwajengea mtizamo mzuri wa maisha ya mbeleni badala ya kuwatupia lawama ambazo baadae zinajenga uadui kati yao na wazazi na jamii.Akikabidhi kombe kwa washindi ambao ni Interspot club ,mwenyekiti wa CCM wilaya ya Arusha Wilfred Soilel amesema kuwa Michezo hujenga hujenga urafiki kati ya vijana ,wanafahamiana pia afya ya mwili inaimarika, pia itamfanya kijana ufahamu wake kuchangamka.

Sambamba ugawaji wa zawadi katika fainali hizo mshindi wa kwanza Intersport club kutoka kata ya Ungalimited, amekabidhiwa Kombe pamoja na Tsh 100,000 ,Mshindi wa pili Mairiva club Tsh 75,000 na mshindi wa tatu ni Black Eagle Tsh 50,000. 

Kiongozi wa Intersport Club akipokea kombe baada ya ushindi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...