Serikali imetakiwa kufungua ofisi za utalii katika kila nchi ambazo zinaleta watalii hapa nchini pamoja na kupunguza viingilio vya wageni wanaotembelea hifadhi zetu za taifa ili kuweza kuongeza idadi ya watalii wanaoingia hapa nchini .

Hayo yamebainishwa na Mbunge wa jimbo la Arumeru magharibi Gibson Olemeiseyeki wakati alipokuwa akiongea na waandishi wa habari alipotembelea katika maonyesho ya utalii ya Karibu fair yanayofanyika ndani ya viwanja ya magereza, jijini Arusha .
wananchi wakiendelea kupata maelezo ya utalii ndani ya banda la Ngorongoro Conservation lililopondani ya maonyesho hayo.

Alisema kuwa serekali inapaswa kufungua ofisi katika kila nchi ambayo inajua inaletawageni hapa nchini ili kuweza kutangaza utalii wetu vizuri,na ili kuweza kupata wageni wengi zaidi ambapo wakiingia kwa wingi watasaidia kuongeza pato la taifa na kupunguza tatizo la ajira kwani vijana wengi wanaweza kujiajiri kupitia utalii pamoja na biashara za utalii .

Alibainisha kuwa ni jambo la ajabu nchi kama Tanzania ambayo inavivutio vingi vya utalii huku ikiwa ni nchi mojawapo ambayo iko katika nchi kumi bora ambazo zinaongoza kwa kuwa na vivutio vya utalii lakini ni nchi ambayo inangiza watalii wachache sana ukilinganisha na vivutio vilivyopo.

“nchi kama Tanzania pamoja na vivutio vyote lakini kwa mwaka tunaingiza watalii milioni moja wakati nchi kama Malaysia kwa mwaka wanaingiza watalii miolini 15 ni jambo la kushangaza alafu ukiwaangalia viongozi wetu badala ya kukaa na kuangalia jinsi ya kufanya ili wataliii waingie na wawe wengi lakini wao wanakaa wanachekelea na wanafanyakazi ya kuongeza ada ya kuingia katika hifadhi zetu kila mara, sasa hii kweli si itakimbiza wageni badala ya kufanya wageni waongezeke kila siku”alisema Olemeiseyeki.
Mbunge wa jimbo la Arumeru magharibi Gibson Olemeiseyeki akipata maelekezo ya huduma zinazotolewa na kampuni ya utalii OSUPUKO nature Paradise iliopo mkoani Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...