Na Samwe Mtuwa – GST

Watalaam watatu wa Taaluma ya Sayansi ya Miamba na Madini kutoka Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) ambao ni Alphonce Michael Bush, Masota Matthew Magigita na Zortosy Mpangile Maganga, wametambuliwa rasmi na Taasisi ya Japan, Oil, Gas, and Metal Cooperation (JOGMEC) ambapo sasa wanaweza kutoa mafunzo ya Utalaam wa Utafiti wa Rasilimali Madini kwa kutumia   Visawe vya Mbali (Remote Sensing) katika nchi za Ukanda wa Kusini mwa Afrika (SADC).

Mmoja wa Wataalam hao ambaye ni Meneja wa kitengo cha Maktaba ya Kumbukumbu ya GST, Masota Magigita, alisema kuwa utambuzi huo umekuja baada ya Taasisi hiyo ya JOGMEC kutoa Mafunzo ya muda mfupi na mrefu, Semina na Warsha mbalimbali  kwa watalaam wa  GST, juu ya kufanya tathmini ya maeneo yenye uwezekano wa kuwepo kwa madini.

“Tathmini hii hufanyika kwa kutumia uchambuzi wa picha zilizopigwa kwa satelite pamoja  na ukusanyaji wa takwimu za Jiosayansi baada ya kufanya kazi za ugani (field work) ili kuboresha kanzidata ya Taasisi,” alisema Magigita.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...