Tanzania Network Information Centre (tzNIC) au Rajisi ya dot tz ni kampuni inayoendesha na kusimamia rasilimali ya nchi (dot tz) kwa ajili mawasiliano kupitia mtandao wa Intaneti. tzNIC inapenda kuuarifu umma wa watanzania kuwa imetenga siku za Jumatatu (27 Juni 2016) na Jumanne (28 Juni 2016) kutoa elimu kwa umma juu ya kazi zake, manufaa ya matumizi ya majina ya kikoa cha dot tz (.tz domain names) na namna bora ya kuhama kutoka matumizi ya majina mengine ya vikoa kama dot com na dot org kwenda kikoa cha dot tz. Katika kipindi hicho tzNIC pia itapokea maoni mbalimbali juu ya uboreshaji  wa huduma zake na nini kifanyike ili watanzania wengi wasajili na kutumia majina ya kikoa cha dot tz kwa ajili ya biashara zao, huduma zao na matumizi binafsi. 
Tukio hili litafanyika katika ukumbi wa mikutano wa tzNIC, Ghorofa ya 8, LAPF Millennium Towers, Kijitonyama, Dar es Salaam kuanzia saa 3 mpaka saa 10 jioni. Kabla ya tukio hili tzNIC itatoa maelezo ya utangulizi kupitia kipindi cha Jambo Tanzania (TBC) siku ya Ijumaa (24 Juni 2016) au Jumatatu (27 Juni 2016) asubuhi. 
Kwa wale wa mikoani na watakaoshindwa kufika wanaweza kutupigia simu (022 2772659 au 022 2772660) au kutuandikia barua pepe kupitia manager@tznic.or.tz) au info@tznic.or.tz
 WOTE MNAKARIBISHWA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...