Kikosi
cha DarCity Veterans, kinachoongozwa na Mwanasoka wa zamani, Tippo
Athuman Shaaban "Zizzou" (Wa nne kulia waliosimama) kikiwa katika picha
ya pamoja, kabla ya mchezo wao wa kirafiki dhidi ya Timu ya Boko Beach
Veretans (BBV), uliopigwa Julai 24, 2016 kwenye Uwanja wa BBV, Boko
Jijini Dar es salaam. Mchezo huo uliowakutanisha pamoja wakombwe mbali
mbali wa Soka nchini enzi hizo na sasa, ulikuwa ni wa burudani ya aina
yake kutokana na uwezo mkubwa wenye ufundi wa hali ya juu ulioonyeshwa
na wakongwe hao, ikiwa ni sehemu ya kuwahamasisha vijana wanaochipukia
na hasa wale wenye vipaji vya Mchezo wa Soka kuupenda mchezo huo na
kuucheza kwa utaalam wa hali ya juu, kwani mchezo huo ni Ajira na ni
burudani pia. Mchezo huo ulimalizika kwa Timu ya DarCity Veterans
kuwachapa Boko Beach Veretans (BBV) Bao 3-0, Mabao mawili yakiwekwa
kimiani na Mshambuliaji Machachari wa DarCity, Juma Kaseja na huku moja
likitupiwa na Kiugo mchezeshaji, Salvatory Edward baada ya kupata krosi
nzuri kutoka kwa Akida Makunda. Pichani toka kulia waliosimama ni Kassa
Mussa, Madaraka Seleman Kibode "Mzee wa Kiminyio", Salvatory Edward,
Tippo Athuman, Ally Mpemba, Maalim Chomba, Idd Seleman Kibode na Meneja
wa Timu ya DarCity, Ernest Nyambo. Waliochuchumaa toka kulia ni, Akida
Makunda, Macocha Moshi Tembele, Shila Mjema, Shaban Kado, Juma Kaseja,
Richardson Sakala, Ally Kakima pamoja na Zubeiry Katwila.
Kikosi cha Boko Beach Veretans (BBV) chini ya Nahodha wake Mabe (kulia waliosimama).
Mshambuliaji machachari wa DarCity Veterans, Shaban Kado akichuana vikali na mabeki wa timu ya Boko Beach Veretans (BBV), wakati wa Mchezo wa kirafiki, uliopigwa Julai 24, 2016 kwenye Uwanja wa BBV, Boko Jijini Dar es salaam .
Akida Makunda wa DarCity Veterans, akiwa katika ubora wake, mbele ya wapinzaji wake.
Kiungo Mnyambuliko wa DarCity Veterans, Tippo Athuman Shaaban "Zizzou" akionyesha utaalam wake, katika mtanange huo wa kuvutia uliopigwa Julai 24, 2016 kwenye Uwanja wa BBV, Boko Jijini Dar es salaam .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...