Wafanyabiashara wakubwa na wadogo nchini wametakiwa kuchangamkia fursa za kujitangaza kibiashara mtandaoni ambazo hazina gharama zozote kwa mfanyabiashara. Hayo yameelezwa na Bwana Tushar Sharma kutoka kampuni ya Leo Leo inayotoa huduma hizo.

Katika mahojiano maalumu na mtandao huu jijini Dar es Salaam, Bwana Tushar alisema ‘tumefungua mtandao mpya ambapo mfanyabiashara yoyote anaweza kujiunga na kutangaza biashara yake, bila gharama zozote. Pia na nafasi ya kipekee kwa watanzania kujipatia bidhaa mbalimbali zinazouzwa na wafanyabiashara hao’

Kuhusu ukubwa wa biashara ambazo zinaruhusiwa katika mtandao huo, Bwana Tushar alisema ‘Hakuna kigezo cha ukubwa wa mtaji wala aina ya biashara, mtandao wetu wa www.leoleo.co.tz hauna ubaguzi wowote, unamruhusu mtu yoyote hata awe na biashara kubwa au ndogo kiasi gani, unajiunga na kutangaza biashara yako.’

Hizi ni habari njema kwani, miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la watumiaji wa mtandao wa internet nchini Tanzania. Inakadiriwa kuwa kuna watumiaji wa Internet kiasi cha milioni kumi na moja nchini, hivyo hawa wote wana nafasi ya kufikiwa na biashar yako bila kulipia gharama zozote. 
Mtandao huu umekuja wakati muafaka ambapo, kumekuwa na upungufu wa ajira nchini, hivyo ni fursa nzuri kwa vijana kujiari kwa kufanya biashara kupitia mtandao wa Leo Leo. Unaweza kutembelea mtandao huo hapa (hyperlink www.leoleo.co.tz) au kutazama kurasa zao za mitandao ya kijamii hapa Facebook (www.facebook.com/leoleotanzania), Instagram (www.instagram.com/leoleotanzania) au Twitter (www.twitter.com/leoleotanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...