Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Samuel M. Nyantahe (Pichani)kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC).
Taarifa ya Katibu
Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa Uteuzi huu umeanza tarehe 20
Julai, 2016.
Kabla ya uteuzi
huo Dkt. Samuel M. Nyantahe alikuwa Mwenyekiti wa Shirikisho la Wenye Viwanda
Tanzania (CTI).
Dkt. Samuel M.
Nyantahe anachukuwa nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Chrisant Majiyatanga
Mzindakaya ambaye amejiuzulu wadhifa huo.
Gerson
Msigwa
Kaimu
Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dodoma
25 Julai,
2016.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...