Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za rambirambi Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Theophil Makunga kutokana na kifo cha Joseph Senga – Mpigapicha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima.

Rais Malinzi amepokea taarifa za kifo cha mwandishi huyo mwandamizi wa habari aliyebobea kuripoti habari za aina mbalimbali ikiwamo za michezo nchini kilichotokea jioni ya Julai 27, 2016 huko India, alikokuwa akipatiwa matibabu ambako habari za kifo chake zilianza kusambaa usiku wa kuamkia jana Julai 28, 2016 kabla ya kuthibitishwa na Mhariri Mtendaji wa Free Media, Neville Meena.

Salamu za rambirambi za Rais wa TFF Malinzi pia zimekwenda kwa familia ya marehemu Joseph Senga, ndugu, jamaa na marafiki na kuwataka kuwa na moyo wa subira wakati huu mgumu wa msiba wa mpendwa wao.

Malinzi alimwelezea Joseph Senga, wakati wa uhai wake alikuwa na mchango mkubwa katika tasnia ya habari za michezo akitoa mawazo yake hivyo ameacha alama ya ucheshi, kujituma na uwajibikaji katika kufanikisha kazi zake katika gazeti la Tanzania Daima na wakati fulani magazeti ya Kampuni ya New Habari House 2006.

Mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya marehemu Joseph Senga mahala pema peponi.

Bwana alitoa, Bwana alitoa, jina la Bwana lihimidiwe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...